Uzinzi Mungu ametuonya tusi zini. Katika
Kutoka 20:14 imeandikwa,
"usizini".
Kumwacha mke wako au mume wako na kuoa mtu mwingine yaweza kuwa halali kwetu lakini kwa Mungu ni dhambi.
Luka 16:18 inasema
"Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini;
naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini." Kutamani mtu asiye mume au mke wako nikuzini katika
Mathayo 5:27 -28 "Mmesikia kwamba imenenwa, usizini; lakini mimi nawaambia, kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini moyoni mwake."
Yesu alimchukulia vipi mwanamke aliyeshikwa akizini?
Yohana 8:10-11 Inasema,
" Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia mwanamke, wako wapi wale washitaki wako?
je! hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia? akamwambia, hakuna Bwana.
Yesu akamwambia wala mimi sikuhukumu. Endazako;
wala usitende dhambi tena." Nimapenzi ya Mungu tusizini. Imeandikwa katika
1Wathesa 4:3 "Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, muepukane na usherati."
Yes, dunia inahitaji kizazi bora ili iendane na mfumo sahihi wa maadili
0 comments:
Post a Comment