Pages

Subscribe:

Thursday, 15 September 2016

Hatareeeeeee kwa Vijana

Uzinzi Mungu ametuonya tusi zini. Katika
Kutoka 20:14 imeandikwa,
"usizini".

Kumwacha mke wako au mume wako na kuoa mtu mwingine yaweza kuwa halali kwetu lakini kwa Mungu ni dhambi.

Luka 16:18 inasema
"Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini;
naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini." Kutamani mtu asiye mume au mke wako nikuzini katika

Mathayo 5:27 -28 "Mmesikia kwamba imenenwa, usizini; lakini mimi nawaambia, kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini moyoni mwake."
Yesu alimchukulia vipi mwanamke aliyeshikwa akizini?

Yohana 8:10-11 Inasema,
" Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia mwanamke, wako wapi wale washitaki wako?
je! hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia? akamwambia, hakuna Bwana.

Yesu akamwambia wala mimi sikuhukumu. Endazako;
wala usitende dhambi tena." Nimapenzi ya Mungu tusizini. Imeandikwa katika

1Wathesa 4:3 "Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, muepukane na usherati."

Yes, dunia inahitaji kizazi bora ili iendane na mfumo sahihi wa maadili

0 comments:

Post a Comment