Pages

Subscribe:

Tuesday, 9 February 2016

WORLD WAR

Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Shirikiano za kijeshi katika Ulaya mwaka 1915. Nyekundu: Mataifa ya Kati; kijani: Mataifa ya Ushirikiano; njano: mataifa yasiyoshiriki vita Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia:

1.Mifereji huko Verdun (Ufaransa) baada ya kulimwa kwa mizinga mikubwa;
2. Ndege za kijeshi na faru za kwanza;
3. bunduki ya mtombo na manowari Ramani ya dunia ikionyesha nchi na maeneo yaliyoshiriki katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia.
Kijani: Mataifa ya Ushirikiano; njano: Mataifa ya Kati; nchi zisizoshiriki kwa rangi ya kijivu Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia ilikuwa vita iliyopigwa kuanzia mwaka 1914 hadi 1918. Mataifa wapiganaji yalikuwa Ujerumani, Austria-Hungaria, Bulgaria na Uturuki (ziliitwa "Mataifa ya Kati") kwa upande mmoja dhidi ya Ufaransa, Urusi, Uingereza, Italia, Marekani na nchi mbalimbali zilizoshirikiana nazo (zilitwa "Mataifa ya Ushirikiano"). Vita hii ilianza katika Ulaya ikapanuka haraka hadi Mashariki ya Kati, Afrika na Asia ya Mashariki ikasababisha kifo cha takriban watu milioni tisa. Yaliyomo 1 Sababu na matokeo 2 Hali kabla ya vita 3 Mwanzo wa vita 4 Vita katika nchi mbalimbali 5 Vita katika makoloni 6 Mwisho wa vita 7 Mkutano wa Paris 8 Vita ya kwanza ya dunia? 9 Tanbihi 10 Marejeo 11 Viungo vya nje 11.1 Ramani hai Sababu na matokeoEdit Sababu yake ilikuwa mashindano makali kati ya mataifa ya Ulaya kuhusu kushika nafasi ya kipaumbele barani Ulaya na duniani kote. Matokeo yake yalikuwa mwisho wa kipaumbele cha Ulaya duniani na kupanda ngazi kwa Marekani, mapinduzi katika nchi mbalimbali, mwisho wa falme za Ujerumani, Austria na Urusi pamoja na mwanzo wa utawala wa kikomunisti katika Urusi, mwisho wa Dola la Austria-Hungaria na wa Dola la Uturuki la Kiosmani pamoja na mwisho wa ukoloni wa Kijerumani duniani. Katika Ulaya nchi mpya zilijitokeza kama vile Chekoslovakia, Finland, Latvia, Estonia na Yugoslavia pamoja na nchi za zamani zilizotokea tena katika uwanja wa kimataifa ndizo Austria, Hungaria, Lithuania na Poland. Hali kabla ya vitaEdit Sehemu kubwa ya Ulaya iliwahi kuwa na kipindi kirefu cha amani tangu vita kati ya Ufaransa na Ujerumani mnamo 1870-1871. Mataifa ya Ulaya yalikuwa na mfumo wa mikataba na mapatano kati yao yaliyolenga kuhakikisha uwiano wa mataifa. Mataifa makubwa ya Ulaya yalikuwa Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Urusi na Italia. Hali ilikuwa tofauti katika Kusini-Mashariki mwa bara hilo. Hadi nusu ya pili ya karne ya 19 sehemu kubwa ya Balkani ilitawaliwa na Milki ya Osmani iliyokuwa milki ya Kiislamu ya kutawala Wakristo wengi. Milki hii iliendelea kudhoofika wakati wa karne ya 19. Nchi mbalimbali zilijitenga na kupata uhuru, kama vile Ugiriki, Serbia, Bulgaria na Romania. Nchi hizi mpya zilipigana kivita kati yao na Milki ya Osmani hadi mwaka 1912. Mwanzo wa vitaEdit Vita Kuu ilianza kutokana na ugomvi kati ya Austria-Hungaria na Serbia. Kutokana na muundo wa mikataba ya kusaidiana kati ya nchi za Ulaya mwanzo huo ulisababisha mfululizo wa hali ya vita kati ya mataifa, na mengine ya Balkani yalitafuta uhuru wao. Tarehe 28 Juni 1914 katika mji wa Sarayevo, Bosnia, mwana wa Kaisari wa Austria aliyekuwa mfalme mteule aliuawa pamoja na mke wake na mgaidi Mserbia mwanachama wa kundi la "Mkono Mweusi" lililopinga utawala wa Austria-Hungaria katika Bosnia. Austria ilidai Serbia ifuate masharti makali katika uchunguzi wa tendo lile. Serbia ilipokataa sehemu ya masharti, Austria ilitangaza hali ya vita dhidi ya Serbia tarehe 28 Julai 1914. Agosti ya 1914 iliona kupanuka kwa vita hii: Warusi walikuwa na mkataba wa usaidizi na Serbia wakatangaza hali ya vita dhidi ya Austria-Hungaria. Hapo wakaingia Wajerumani waliokuwa na mapatano ya usaidizi na Austria-Hungaria wakitangaza hali ya vita dhidi ya Urusi. Urusi kwa upande wake ulikuwa na mkataba wa kusaidiana na Ufaransa, hivyo hali ya vita ikajitokeza pia kati ya Ufaransa na Ujerumani. Uingereza ulijiunga na vita baada ya Wajerumani kuanza kuingia eneo la Ubelgiji kwa shabaha ya kuvuka haraka ili wavamie Ufaransa Kaskazini. Kuanzia Oktoba 1914 Milki ya Osmani (Uturuki) ilijiunga na vita kufuatana na mkataba wake wa siri na Ujerumani. Mwaka 1915 Italia ilijiunga na Wafaransa na Waingereza kwa kushambulia Austria-Hungaria, ingawa awali ilikuwa na mkataba na dola hilo. Vita katika nchi mbalimbaliEdit Vita ilipigwa kwa ukali miaka ya 1914-1918. Wajerumani waliingia ndani ya Ufaransa lakini walikwama kabla ya kufikia mji mkuu wa Paris. Kwa muda mrefu mstari wa mapambano ulibaki palepale. Katika Mashariki Wajerumani walifaulu kurudisha mashambulio ya Kirusi na kuteka sehemu za Urusi. Katika Kusini mwa Ulaya Waustria walifaulu kwa shida kubwa kuteka Serbia na Montenegro pamoja na Albania. Waturuki walishindwa kwa ujumla katika mashambulio yao dhidi ya Warusi katika eneo la Kaukazi na dhidi ya Waingereza katika Misri. Lakini walifaulu kuzuia Waingereza wasifike Uturuki penyewe. Waingereza walipeleka jeshi katika Irak ya kusini wakafaulu kuwarudisha Waturuki hadi kaskazini ya nchi hii. Vita katika makoloniEdit Vita ilienea haraka baharini na katika makoloni ya Ujerumani yaliyovamiwa na Waingereza, Wafaransa, Afrika Kusini na Japani. Makoloni yalikuwepo Afrika na kwenye visiwa vya Pasifiki pamoja na China. Ujerumani ilikuwa na vikosi vya kijeshi katika makoloni ya Afrika na pia huko Qingdao nchini China. Kwa ujumla makoloni yote yasiyokuwa na jeshi yalitekwa na mataifa ya ushirikiano bila mapigano. Afrika ya Kusini-Magharibi ya Kijerumani ilivamiwa na Afrika Kusini na jeshi la ulinzi la Kijerumani likajisalimisha mnamo Julai 1915. Kamerun ilivamiwa na Ufaransa na Uingereza kutoka makoloni yao ya Nigeria na Afrika ya Kati ya Kifaransa. Jeshi la ulinzi likajisalimisha katika Februari 1916. Afrika ya Mashariki ya Kijerumani ilikuwa mahali pa mapigano yaliyoendelea kwa miaka yote ya vita. Jeshi la Ulinzi wa Kijerumani chini ya uongozi wa Paul von Lettow-Vorbeck lilifaulu kutetea eneo la koloni dhidi ya mashambulio ya kwanza ya Waingereza kutoka Kenya hadi 1916. Kwenye Novemba 1914 jeshi la askari 8,000

0 comments:

Post a Comment