Pages

Subscribe:

Saturday, 14 February 2026

SILAHA KAMILI ZA MUNGU

🔥 SILAHA ZA KIROHO ZA KUSHINDA NGUVU ZA GIZA

Na: Ev ELIMELECK S NDASHIKIWE 

UTANGULIZI
Wapendwa, vita tuliyonayo si ya damu na nyama! Adui yetu si jirani, si binadamu — bali ni falme za giza. 
      Kama inavyoandikwa katika Biblia (WAEFESO 6:12), tunashindana na falme na mamlaka za giza.


Lakini nina habari njema leo 

    HATUJAPEWA ROHO YA WOGA! Tumepewa mamlaka na silaha za ushindi!

1️⃣ MKANDA WA KWELI – SIMAMA KATIKA UKWELI
Uongo ni silaha ya shetani.
      Lakini ukweli ni silaha ya Mungu.
Yesu alisema, “Mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka huru.”

Ukiishi katika ukweli:
Huna hofu
Huna mashaka
Adui hana pa kukushika

🔥 Sema: Ninasimama katika ukweli wa Mungu!

2️⃣ DIRII YA HAKI – LINDA MOYO WAKO

Dhambi humpa adui nafasi. Lakini haki hufunga milango ya giza.
Unapotembea katika utakatifu, unavaa ulinzi wa mbinguni.
🔥 Sema: Ninavaa dirii ya haki leo!

3️⃣ NGAO YA IMANI – ZIMA MISHARE YA MOTO

Mashambulizi ya adui huja kwa njia ya:
Hofu
Mashaka
Maneno mabaya
Ndoto za kutisha

Lakini imani inazima mishale yote ya moto!
Kama inavyoandikwa katika Waefeso 6:16 — ichukueni ngao ya imani.
🔥 Sema: Imani yangu haiwezi kuzimwa!

4️⃣ UPANGA WA ROHO – NENO LA MUNGU

Hii ndiyo silaha ya kushambulia!

Yesu alipokuwa akijaribiwa jangwani, alishinda kwa kusema, “Imeandikwa!”
Neno la Mungu linavunja laana, linaangusha ngome, na kufungua vifungo!
 2 WAKORINTHO 10:4, silaha za vita vyetu zina nguvu katika Mungu kuangusha ngome.

🔥 Tangazia hali yako: IMEANDIKWA!

5️⃣ MAOMBI – NGUVU YA SIRI

Hakuna ushindi bila maombi.
Maombi ni mawasiliano na mbingu.
Maombi hubadilisha hali.
Maombi huleta moto wa Roho.

🔥 Omba bila kukoma!

HITIMISHO: USHINDI NI WAKO!
        Wapendwa, huna haja ya kuogopa wachawi wala kuzimu.
Yesu tayari alishinda msalabani!

Simama. Vaa silaha. Tumia mamlaka yako.
🔥 Sema kwa sauti kubwa:
Mimi ni mshindi!
Nimeshinda kwa damu ya Yesu!
Hakuna nguvu ya giza itakayenishinda!

Nipigie Kwa

+255 698 52 50 10

0 comments:

Post a Comment