Pages

Subscribe:

Tuesday, 18 October 2016

KUOKOKA

Watu wengi wamekua wakijiuliza kuhusu kuokoka ni nini,
jamii nyingine wamekua wakipinga jambo la kuokoka hapa duniani kana kwamba wataweza kutenda jambo wakiwa marehemu ambalo litawafanya waokoke.

Lakini kuokoka wanadamu tunaokoka hapa hapa duniani maana hatuwezi kufanya chochote tukiwa wafu hivyo kwa maamuzi ya leo unaweza kuokoka, kwa matendo yako ya sasa unaweza kuokoka na sio baadae baada ya kufa.

*Kuokoka ni kumwamini YESU KRISTO.
Yohana 1:12 -13
‘’Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake;
waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa MUNGU.

‘’ Kumwamini YESU ni kumkubali YESU na pia kumtegemea kwa kila kitu, na yeye alisema kwamba sisi bila yeye hatuwezi kufanya lolote hata lile lililo dogo kabisa.

Matendo 16:30-31
Biblia inasema
‘’ kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka?
Wakamwambia,
Mwamini BWANA YESU, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako. ‘’

*Tukimwamini BWANA YESU tunakuwa na ROHO MTAKATIFU ambaye hutufanya kuchukia dhambi kwani bila ROHO MTAKATIFU hakuna awezaye kuacha dhambi.

BIBLIA katika
Yohana 3:3
‘’YESU akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa MUNGU. ‘’

*Kuzaliwa mara ya pili ni
1: Kumwamini YESU.
2: Kubatizwa .
3: Kuwa na ROHO MTAKATIFU.

Yohana 3:17-18’’
Maana MUNGU hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa MUNGU.

‘’ Tunaokoka hapa hapa duniani kwa sababu ‘’
Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya KRISTO amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama!
Yamekuwa mapya. ‘’
- 2 Korintho 5:17.

*Ndugu ukiamua kuokoka usirudi nyuma maana unaweza ukapoteza wokovu wako.
Luka 9:61-62'' Mtu mwingine pia akamwambia, BWANA, nitakufuata; lakini, nipe ruhusa kwanza nikawaage watu wa nyumbani mwangu.
YESU akamwambia,
Mtu aliyetia mkono wake kulima, kisha akaangalia nyuma, hafai kwa ufalme wa MUNGU.''

*Watu wengine huogopa kuacha dhambi eti kwa sababu shetani atawatesa kwa sababu wamewahi kuingia maagano naye ya kishetani huo ni uongo.

Maana YESU akikuokoa anakuhamisha kutoka katika kila agano lako na shetani na kuanzia muda hu unakua mtoto wa MUNGU ambaye huwezi kurogwa tena maana mamlaka ya BABA yako wa mbinguni uliyeamua kumpa maisha yako ni kuu sana na hakuna anayeweza kukudhuru tena

na BWANA YESU atakuwa ndiye anayekuchunga 
Zaburi 23:1’
’ BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. ‘’ .

*Ndugu duniani hapa tunapita tu maana hata kama ukiishi miaka 98 hapa duniani lakini ni bure kabisa kama utapotelea motoni baada ya kufa kwa hiyo bora kumpa YESU maisha yako na utakuwa huru kabisa pia utapata uzima sasa na baadae uzima tele.

YESU anasema katika
Yohana 10:10b’’
mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele. ‘’.

ndugu dunia hii tuliikuta na tutaiacha hivyo ni heri kwa sasa kuishi maisha ya kumcha MUNGU.

Neno la MUNGU linakushauri kwamba ‘’

Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia.
Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.
Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya MUNGU adumu hata milele. ‘
’-1 Yohana 2:15-17

Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho,

amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU
ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.

MUNGU akubariki sana.

Ni Mimi ndugu yako

Ev. Elimeleck Ndashikiwe

+255767445846
+255715445846

3 comments:

  1. Ishi kikamlifu hivo hivo mtumishi wa Mungu mpaka Mungu atakapojitwalia utukufu

    ReplyDelete
  2. Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.

    Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.

    Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.

    Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.

    Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.

    Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
    dawnacuna314@gmail.com

    ReplyDelete
  3. Uchawi wa mapenzi wa Dkt. Dawn hufanya maajabu kweli.

    Niliwasiliana na Dkt. Dawn wakati uhusiano wangu ulipovunjika kabisa. Mpenzi wangu wa zamani alikuwa ameniacha na kunizuia kwenye mitandao yote ya kijamii. Nilivunjika moyo na kupoteza tumaini. Baada ya kushauriana na Dkt. Dawn, kila kitu kilibadilika. Mpenzi wangu wa zamani alirudi peke yake, akaomba msamaha kwa dhati, na akaomba msamaha. Leo, tunaishi pamoja kwa furaha, na hata tuna mtoto.

    Maneno hayatoshi kuelezea jinsi ninavyoshukuru. Kutokana na uzoefu wangu, naweza kusema kwa ujasiri kwamba Dkt. Dawn ni halisi, anayetegemewa, na mwenye nguvu. Ikiwa unakabiliwa na hali yoyote ngumu maishani mwako hivi sasa, Dkt. Dawn anaweza kukusaidia.
    ANAWEZA KUKUSAIDIA KWA MATATIZO YAFUATAYO:
    Kurudisha ndoa na mahusiano yaliyovunjika
    Kuvutia mafanikio na ukuaji katika biashara
    Matatizo ya uanaume, utasa, na ukosefu wa watoto
    Kurejesha mali zilizoibiwa au zilizopotea
    Kurudisha kazi zilizopotea au fursa za kazi
    Kinga dhidi ya uchawi na macho mabaya
    Hirizi za mvuto
    Kutatua migogoro ya ardhi na mali
    Kuwafanya wapenzi kutimiza ahadi zao
    Kushinda kesi mahakamani, na mengine mengi
    Huu si ulaghai — ni ushuhuda kutoka kwa uzoefu.
    Kwa maelezo zaidi, wasiliana naye moja kwa moja kwenye WhatsApp. +2349046229159
    dawnacuna314@gmail.com

    ReplyDelete