Pages

Subscribe:

Friday, 2 July 2021

KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU

MH: PASTOR TARIMO
SOMO:   AINA ZA KARAMA ZA ROHO NA HUDUMA 
    

       Bwana Yesu asifiwe sana ndugu yangu mpendwa msomaji wangu, MUNGU wangu wa Mbinguni akubariki sana kwa kuendelea kuwa nami.

              1Korintho 12:1............ Basi ndugu kwa habari ya karama ...................

   Mtume Paulo anaongelea kwa habari ya KARAMA ZA ROHO ambazo Mungu ameziachilia kwa kanisa ili tu kuukamilisha utumishi kwa watu  wake katika ulimwengu wa Roho na ule wa mwili.

            Ukiendeloea kusoma hadi mstr wa 11 utakutana na namna karama hizi za Roho zinavyofanya kazi kwa masaidizano chini ya uongozi wa ROHO MTAKATIFU.

AINA ZA KARAMA ZA ROHO
         Ziko aina mbalimbali sana za Karama za Roho, lakini katika karama zote hizo zilizo kuu ni karama tisa.
       Aina hizi za karama tunakutana nazo katika kitabu hiki cha 1Kor 12:8

1. Neno la Maarifa
           Aina hii ya karama  inasimamia juu ya utambuzi katika kuwahudumia watu,  mtumishi anaweza kutambua uhitaji wa mtu juu ya kile kinachomsibu kiroho na kimwili.
         Roho wa Mungu atahakikisha anakuonesha kwa ishara kupitia mwili wako mwenyewe.

    Mfano unaweza kujisikia unaumwa kichwa wakati ukiwa ktk huduma,  kumbe Mungu anakuonesha kuwa kuna mtu pembeni anasumbuliwa na kichwa.

2. Neno la Hekima
            Aina hii ya karama inasimamia juu ya utatuzi ktk masuala malimbali ya kiroho na kimwili katika maamuzi.      Mfano wa jambo hili tunaliona kwa mtumishi wa MUNGU Mfalme Suleimani alipoletewa mtoto aliyekuwa akigombewa na wanawake wawili makahaba  
 1Wafalme 3:16-27 utakutana na habari hii.

3. Karama ya Imani
             Aina hii ya Karama inasimamia misingi ya namna Wokovu ulivyojengeka na kujengwa ndani yake.
Maana chanzo cha imani huja kwa kusikia, itategemea umesikia nini na  kwa nani.

Isipokuwa chanzo cha imani ya KRISTO huja kwa kusikia NENO la Kristo mwenyewe.
.............................. IMANI wakati mwingine ni kitu anachopewa mtu kama karama.

4. Karama ya Kinabii na Huduma ya Kinabii
                    =Karama ya kinabii huwa sio ya kudumu, Mungu huiachilia ndani ya mtu maalumu, kwa wakati maalumu na kwa kusudi maalumu.

                    =Huduma ya kinabii hii huwa ni ya kudumu na huwa ni kama ofisi maalumu kwa kazi hiyo.

5. Karama ya Kuponya
                 Aina hii ya karama huwa inasimamia juu ya uwezo katika kuponya, kuwa na juhudi na nguvu ya imani juu ya NGUVU NA UWEZA ULIO KATIKA MUNGU kupitia jina la YESU KRISTO.


6. Matendo ya Miujiza
7. Kupambanua Roho
              si kila roho inatokana na Mungu

8. Aina za Lugha na
9. Tafsiri za Lugha.

......................Karama zina tabia tofauti tofauti ambazo haziwezi kufanana ingawa zinaweza kuingiliana katika utendaji kazi maana zinaongozwa na Roho yule yule mmoja wa MUNGU.

NB;
         KATIKA UTUMISHI WA KUTUMIKIA KWA AJILI YA KRISTO, kuna mikoba mitatu ya muhimu na ya lazima sana ambayo hutakiwi kuikosa.
                .Huduma tano EFES 4;11-12
           .Karama Tisa  1KOR 12;8-10
           .Matunda Tisa  GALAT 5;22-23

TUTAENDELEA NA KIPENGELE CHA HUDUMA.......................

MUNGU WANGU WA MBINGUNI AZIDI KUKU INUA 

Karibu sana katika ibada zetu zinazoendelea hapa kanisani 

PENTECOST TABARNACLE OF PRAISE Kisanga "B" Wazo!

0 comments:

Post a Comment