AINA ZA KUFUNGA.
Zipo aina tano ( 5 ) za kufunga.
1. TOTAL FAST (FUNGA KAVU).
Absolute fasting (Funga iliyo sahihi)
Hii ni funga ya kutokula chakula kabisa wala kunya maji kwa siku zisizo zidi tatu (3)
kama (Esta 4:16).
b. Supernatural Fasting (Funga ya Kiungu).
Funga ya kutokula chakula kabisa wala kunywa maji kwa siku zaidi ya tatu (3) kama Musa
(Kumb.9:9 & 9:18) kwa siku 40.
2. PARTIAL FASTING (FUNGA NUSU)
a. Yohana Mbatizaji aliamua kufunga maisha yake yote akila asali na Nzige tu. Dan. 10:2-3
Kuacha kula aina maalumu ya vyakula ambavyo ungevipenda.
b. Funga ya milo miwili au mmoja kwa siku.
c. Funga ya kawaida (Normal fasting).Kunya maji tu.
3. FUNGA YA KULAZIMISHWA (IMPOSED FAST).
Matendo 28:1
Safari ya Paulo akielekea Rumi.Kwasababu ya misukosuko ya mawimbi majini watu wanashindwa kula.
Pia kama mtu anaumwa unakosa hamu ya chakula.Mala nyingine tunapata misukosuko kama sehemu ya Maisha kiroho pia.
4. FUNGA YA WAZI/KANISA, HADHARA AU TAIFA.
(PUBLIC AND NATIONAL/CHURCH FASTS).
Hii inakuwa funga ambayo inatangazwa na inakuwa wazi kwa kila mtu.Sio za siri.
Yona 3:6. 5.
Funga ya mtu binafsi Hii hufanywa na mtu mmoja kwa siri na mungu wake hapana anayejua mtu huyo kama amefunga.
SIFA 7 ZA KUFUNGA NA KUOMBA KUNAKOONGEA
1. Huongozwa na roho wa Mungu
Marko 1:12-14,
Yesu aliongozwa na roho kufunga nyikani ndio
maana hakutenda dhambi katika kufunga na kuomba kwake.
2. Lazima iwe katika kweli ya Mungu. Kama funga na kuomba huko hakuko katika
roho hakuwezi kuwa katika kweli kwa kuwa roho wa mungu hatenganishwi na kweli ya Mungu.
2samwel12:16-17
Daudi alijaribu kufunga na kuomba ili motto aliyezaliwa katika zinaa asife hakufanikiwa
kwa kuwa Mungu tayari alisema atakufa hakika.
Hata alipokuwa ameshakufa daudi aliendelea kufunga hii inadhihirisha kuwa hakuwa rohoni kwa sababu alijua anachoomba
siyo mapenzi ya Mungu.
Angekuwa rohoni roho angemjulisha aache kuomba kwa kuwa Mungu amekataa.
3. Lazima uwe mtu wa Mungu uliyeitwa kwa jina lake 1cronicles
(2Nya 7:14a
Hapa tunaona Mungu anadhirisha kuwa si kila mtu wa Mungu ameitwa kwa jina lake. Aliyeitwa kwa jina lake ni Yule aliyezaliwa mara ya pili katika roho mtakatifu
(Yohana 1:11-13) 4.
Lazima funga ifanywe katika unyenyekevu wa hali ya juu wa rohoni.
Mtu anayefunga kwa kiburi cha uzima hawezi kupata matokeo yaliyokusudiwa. Mfano
unafunga ili ujilipizie hasira yako kwa mtu anayekudharau au kutesa, unataka kushindana na wengine,
unataka kuonesha kwamba wewe ni mwamba kanisani kwenu nk.
Isaya 58:3-4)
“Husema mbona tumefunga lakini huoni, mbona tumejitaabisha nafsi zetu lakini huangalii?
Fahamuni siku ya kufunga kwenu mnatafuta anasa zenu wenyewe, na kuwalemea wote watendao kazi kwenu, Tazama
ninyi mwafunga mpate kushindana, kugombana na kupiga ngumi ya uovu” 5.
Lazima ifanywe katika furaha ya roho mtakatifu na siyo kwa kujilazimisha na kunung’unika Ukifunga kama andiko la
Isaya 58:3
inasema (mbona tumefunga lakini huoni,
mbona tumejitaabisha nafsi zetu lakini huangalii?
Hutapata matokeo yaliyokusudiwa. Badala yake fanya funga na maombi yaliyojaa furaha ya roho mtakatifu
Mathayo 6:16-18
“tena mfungapo msiwe kama wanafiki, wenye uso wa kukunjamana, maana hujiumbua nyuso zao ili waonekane na watu kuwa wanafunga,
amini nawaambia wamekwishakupata thawabu yao.
Bali wewe ufungapio jipake mafuta kichwani,
unawe uso ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na baba yako aliye sirini na baba yako aonaye sirini atakujazi” linganisha andiko hilo na
Isaya 58:5 6.
Lazima kufunga kuambatane na kuomba na kuutafuta uso wa bwana 2Nya 7:14, 7.
Lazima kufunga na kuomba kufuate kanuni ya upendo na si ubinafsi. Yaani kumpenda
Mungu na jirani kama nafsi yako mwenyewe.
Matendo ya upendo kwa mungu na watu ni kama
1. hicho ambacho ungekula mpe Yesu ale. Unadhani Yesu anapatikana kanisani?
Hapana, msikie mwenyewe anapatikana wapi katika
Math 25:34-40
“Kisha mfalme akawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, njooni mliobarikiwa
na baba yangu, urithini ufalme muliowekewa tayari tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu kwa maana nalikuwa
na njaa mkanipa chakula, nalikuwa na kiu mkaninywesha, nalikuwa mgeni mkanikaribisha, nalikuwa uchi mkanivika,
nalikuwa mgonjwa mkaja kunitazama, nalikuwa kifungoni mkanijia………………………………………amini nawaambia yoyote mliyowatendea mmojawapo ya hao ndugu zangu walio wadogo mlinitendea mimi”
NB: Linganisha andiko hilo na
Isaya 58:6a, 7
Je, Swaumu niliyoichagua mimi siyo ya namna hii?……………. je siyo kuwagawia wenye njaa chakula chako na kuwaleta maskini waliotupwa nje nyumbani mwako?
Umwonapo mtu aliye uchi umvike nguo, wala usijifiche na mtu mwenye damu moja nawe”
2. Ombea watu wengine kama familia, jamii yako, familia na taifa kwa nguvu ileile unayotumia kuombea mahitaji yako binafsi.
Isaya 58:6,
2Samweli 22: 25-26.
“ kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili, kwa mkamilifu utajionyesha
kuwa mkamilifu, kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi”
Nehemia 1:1-11
jinsi Nehemia alivyolia na kutubu kwa habari ya mabaya yaliyoipata Israel na Yeusalem
hakujali kuwa alikuwa mahali salama.
Danieli 9
jinsi alivyolia kwa Mungu kwa habari ya wayahudi hata kama yeye mwenyewe alikuwa ikulu akiheshimika sana.
Au Ester ambaye alikuwa mke wa mfalme Ahusueoro angeweza kubaki alivyo lakini alifunga na kupomba kwa ajili ya
ndugu zake
SABABU /FAIDA 12 ZA KUFUNGA NA KUOMBA KATIKA KANISA
(MTU AU USHIRIKA)
1. Tunafunga kuonyesha utii kwa neno la Mungu
(Yoeli 2:12)
Biblia kuanzia agano la kale hadi agano jipya inaonyesha umuhimu wa kufunga.
Watumishi wote wa Mungu walikuwa wanafunga katika siku za maisha yao hivyo
unavyofunga unaonyesha utii katika kulifuata neno la Mungu na kuliamini.
Yesu Pia alisema kuwa siku zinakuja ambapo tutalazimika kufunga.
(Mathayo 9:15)
2. Tunafunga ili kujinyenyekeza mbele za Mungu na kupata nguvu na neema yake.
Tunahitaji neema ya Mungu siku zote ili tuweze kuishi, na ili kuipata inatubidi kujinyenyekeza chini ya mkono wake ulio hodari,
Ebrania 4:16, na Yakobo 4:10.
Ezra aliwaamuru watu wafunge ili wapate kujinyenyekeza
mbele za Mungu na kupata neema yake kwa ajili ya taifa lao,
Ezra 8:21. 3.
Tunafunga ili kuomba rehema Yesu alichukua dhambi zetu zote msalabani, inawezekana kuna jambo unaona unashindwa
kuacha na umejaribu sana. Hapo unatakiwa kufunga na kuomba rehema ili Mungu akuwezeshe kushinda. Pia unafunga kuomba rehema kwa ajili ya wengine mfano familia, jamaa na taifa pia.
Daniel alifunga na kuomba rehema kwa ajili ya dhambi za taifa la Israeli na kubeba uovu wao mbele za Mungu. Danieli 9:3-5.
Taifa la Ninawi walifunga na kuomba rehema kwa Mungu kutokana na uovu wao.
Yona 3:5-10 4.
Tunafunga ili katika udhaifu wetu Nguvu ya Mungu ionekane Unapofunga unakuwa umeikana nafsi na kumchagua Mungu,
uankuwa umedhamiria moyoni kutaka kuona nguvu ya Mungu ikionekana na sio nguvu yako.
Zaburi 109:24-28,
2Korintho 12:9-10 5.
Tunafunga kupata msaada wa Mungu katika kukamilisha kusudi lake Viongozi wa
kanisa la Antiokia walifunga na kuomba kabla ya kuwatuma Paulo na Barnabas.
Walifanya hivi ili waweze fanya uchaguzi sahihi chini ya uongozi wa Mungu.
Na Paulo na Barnabas
walikuwa wakifanya hivyo katika miji waliyotembelea kila walipokuwa wanataka
kuchagua viongozi.
Kutokana na jambo hili makanisa yale yalizidi kusonga mbele maana walimshirikisha Mungu kwa kufunga katika maamuzi yao yote.
Matendo 13:3-4, 14:23 6.
Tunafunga wakati wa taabu Mordekai na Esta walitangaza kufunga kwa wayahudi wote pale
ilipofahamika kuwa kuna mpango wa kuwateketeza wayahudi wote, na kupitia kufunga na kuomba huku wayahudi walisalimika.
Ester 4:15-16.
Wakati wa taabu ni wakati wa kufunga na kumlilia Mungu na hakika Mungu ataonekana.
Mfalme Yehoshafati pia alitangaza kufunga pale walipokuwa wamevamiwa na maadui wengi na wao hawakuwa na uwezo
wa kupigana nao
2Nyakati 20.
Tumeona kwa uchache jinsi kufunga kulivyo muhimu katika maisha yetu ya kila siku. 7.
Kufunga hunoa Imani (ili iwe kali) na huongeza ujasiri.
Esta 4:16.
Huyu mama asingefunga alikuwa hana ujasiri
wala imani ya kuingia kwa mfalme kinyume cha sheria – kwasababu adhabu yake ilikuwa ni kifo.
Ndio maana aliomba wayahudi wote walio kuwa shushani wambebe kwa maombi.
8. Kufunga huleta unyenyekevu mbele za Mungu.
Luka 14:11 & 18:14 Ezra 8:21.
Mungu huwapa wanyenye kevu neema,na kuwainua.
(1Petro5:5-6).
Ukitaka kuwa mnyenyekevu mbele za Mungu basi jifunze kuwa mfungaji. 9. Kufunga huongeza/huleta nguvu ya Maombi na kuondoa ukame wa kiroho.
Zaburi 35:13
Kufunga ni kama 4WD ya maombi.
ISAYA 40:31
na Mithali 20:13. 10.
Kufunga hufanya ulimwengu wa roho uwe wazi.
Daniel 10:14.
Baada ya Danieli kufunga siku 21 alianza kuonyeshwa na Mungu mambo ya siku za mwisho
za dunia ambako hata 11. Kukuza kanisa na huduma ya Mungu a. Hili tendo lililofanywa sana na mitume na wafuasi wao.
Mdo 14:22.
Kukua kwa Kanisa la kwanza kulitegemea Maombi ya kufunga.
b. Ushuhuda wa Paulo kuhusu maisha yake.Akafanikiwa sana kwa sababu ya maombi ya kufunga.
2Koritho 6:4-6. 12.
Kutiisha miili yetu ipate kumtii Kristo. Miili yetu siku zote hupingana na Roho Mtakatifu.
Galatia 5:16-17.
nia ya Mwilini uadui dhidi ya Mungu
Rumi 8:7-8
hivyo inabidi tuiitiishe kwa kufunga
1Kor.9:27.
Mungu akubariki mpendwa wangu!
Ni Mimi ndugu yako
Ev. Elimeleck S Ndashikiwe
+255767445846 &
+255715445846




Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.
ReplyDeleteMwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.
Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.
Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.
Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.
Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
dawnacuna314@gmail.com
Uchawi wa mapenzi wa Dkt. Dawn hufanya maajabu kweli.
ReplyDeleteNiliwasiliana na Dkt. Dawn wakati uhusiano wangu ulipovunjika kabisa. Mpenzi wangu wa zamani alikuwa ameniacha na kunizuia kwenye mitandao yote ya kijamii. Nilivunjika moyo na kupoteza tumaini. Baada ya kushauriana na Dkt. Dawn, kila kitu kilibadilika. Mpenzi wangu wa zamani alirudi peke yake, akaomba msamaha kwa dhati, na akaomba msamaha. Leo, tunaishi pamoja kwa furaha, na hata tuna mtoto.
Maneno hayatoshi kuelezea jinsi ninavyoshukuru. Kutokana na uzoefu wangu, naweza kusema kwa ujasiri kwamba Dkt. Dawn ni halisi, anayetegemewa, na mwenye nguvu. Ikiwa unakabiliwa na hali yoyote ngumu maishani mwako hivi sasa, Dkt. Dawn anaweza kukusaidia.
ANAWEZA KUKUSAIDIA KWA MATATIZO YAFUATAYO:
Kurudisha ndoa na mahusiano yaliyovunjika
Kuvutia mafanikio na ukuaji katika biashara
Matatizo ya uanaume, utasa, na ukosefu wa watoto
Kurejesha mali zilizoibiwa au zilizopotea
Kurudisha kazi zilizopotea au fursa za kazi
Kinga dhidi ya uchawi na macho mabaya
Hirizi za mvuto
Kutatua migogoro ya ardhi na mali
Kuwafanya wapenzi kutimiza ahadi zao
Kushinda kesi mahakamani, na mengine mengi
Huu si ulaghai — ni ushuhuda kutoka kwa uzoefu.
Kwa maelezo zaidi, wasiliana naye moja kwa moja kwenye WhatsApp. +2349046229159
dawnacuna314@gmail.com