Pages

Subscribe:

Monday, 8 May 2017

DHIKI KUU DUNIANI

TAIFA LA ISRAELI WAKATI WA DHIKI KUU

Heshima Yarudi Yerusalemu

Watu wengi hufanya makosa pale ambapo hawaangalii na kuchunguza kwa makini yale yanayosemwa kuhusu taifa la Israeli siku za mwisho.

             Kwa vile hawajui au hawaelewi ni yapi yametajwa kuhusu taifa hili,
wao hupata          ugumu kuelewa yale Biblia inasema kuhusu dhiki kuu siku za mwisho.

Pia mengi ya unabii yanayohusu kuenea
(dispensation)  kanisa hayaeleweki na wengi.

Na lile la muhimu sana ambalo halitiliwi maanani ni kurudishwa kwa Yerusalemu katika taifa la Israeli kuwa makao
makuu au mji mkuu wa taifa hili.

Na kuhusu kurudi kwake Kristo mara ya pili, katika

Ufunuo 1:7
"Tazama, yuaja na mawingu; kila jicho litamwona,
na hao waliomchoma; na kabila zote za dunia wataomboleza kwa ajili yake. Naam.
Amina."

Haya tuliyosoma yanasema wazi kwamba lazima waIsraei warudi katika taifa lao ili waweze kuchukua uamuzi fulani maalum kuhusu Kristo aliyesulubiwa,

na kukataliwa kwa wale waliokuwa wake wakati
yeye alipokuja mara ya kwanza.

Mji wa Yeruslemu ni mji wa muhimu kabisa kwani hii ndio ishara moja kuu mwokozi
wetu yesu Kristo alitupa kuhusu mwisho wa kuenea kanisa wakati huu, na mwanzo wa dhiki kuu.

Baada ya kueleza kuharibika kwa mji wa Yerusalemu katika
Luka 19:41-44 na 21:5-6

yeye alitaja kutawanyika kwa wayahudi kote duniani,
kwamba Yerusalemu itakaliwa kimabavu na kuharibiwa na mataifa yasiyo ya kiyahudi:

"Ole wao wenye mimba na wanaonyonyesha katika siku hizo! Kwa kuwa kutakuwa na shida nyingi katika nchi,
na hasira juu ya taifa hili.

Wataanguka kwa ukali wa upanga, nao watatekwa nyara na kuchukuliwa katika mataifa yote;
na Yerusalemu utakanyagwa na mataifa,
hata majira ya mataifa yatakapotimia"
(Lk. 21:23-24).

         Mtume Paulo anasema wakati huu wa waIsraeli kutawanyika ni wakati ambapo
roho zao zitazidi kuwa ngumu,
na kwao wasio na imani kuwa ni wakati wao kupokea kwa wingi ujumbe wa injili.

Ugumu katika roho za wayahudi umefikia kiwango ambapo mpaka wale wasio na imani wamepokea.

Hata hivyo wote katika taifa la Israeli watapokea wokovu kwa vile imeandikwa katika
Warumi 11:25-26:
"Kwa maana, ndugu zangu sipendi msijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili;
ya kwamba kwa sehemu ngumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa mataifa uwasili.

Hivyo Israeli wote wataokoka;
kama ilivyoandikwa, mwokozi atakuja kutoka Sayuni;
atamtenga Yakobo na maasia yake."

Luka 21:24
hahitaji tu wakati ule ambapo Yerusalemu haitakuwa mji ulionyanyaswa,
bali inazungumzia wakati ambapo kazi ya kuenea kwa kanisa itakuwa imekwisha.

Ni jambo la muhimu kuelewa vyema nakujua
ni yapi yanatokea katika mji wa Yerusalemu chini ya wayahudi ili kuweza kufahamu vyema yale yanayotajwa kuhusu nyakati za mwisho
Lk. 12:54-56.

Wakati taifa la Israeli lilipopata mamlaka ya kuwa taifa mwaka wa 1948, taifa hili lilipewa madaraka juu ya sehemu ndogo tu,
ambayo ni sehemu mpya ya Yerusalemu.

Hii ilikuwa ishara kwamba nyakati za mwisho zilikuwa zinakaribia.

Tukio la muhimu sana lilitokea pale mwaka wa 1967 pale sehemu ya Yerusalemu ambayo ni mji wa kale ambako
kuna Zion na Temple Mount,

na hata sehemu ya mashariki ya Yerusalemu
kuchukuliwa kwa nguvu kutoka Jordan wakati wa vita vikali vya siku sita (Six-day War.)

Hadi wakati huo,
tayari Yerusalemu ilikuwa imejengwa upya, na hii ingefuatwa na Yerusalemu kufanywa kuwa makao makuu ya kisiasa
katika taifa hili la Israeli.

Ni bora kukumbuka hapa kwamba mara ya mwisho Yerusalemu palikuwa ni mahali
ambapo ni mji huru ilikuwa ni pale karne ya sita.

Pale wakati Kristo alipokuwa hapa duniani, bendera iliyokuwa ikipepea Yerusalemu ilikuwa ni bendera ya ufalme wa Kirumi.

Mnamo Agosti 1980,
Waziri mkuu wa Israeli
Menachim Begin
alitangaza wazi kwamba Yerusalemu ndio mji mkuu usioweza kugawanywa wa taifa la Israeli,

na hapo akahamisha makao yake makuu kutoka Tel-Aviv hadi hapa Yerusalemu.

Miaka miwili baadaye,
baraza lake lote la mawaziri lilihamia Yerusalemu.

Hapa basi Yerusalemu ukawa mji mpya ambao ni makao makuu ya kisiasa ya taiafa hili la Israeli.

Lile ambalo lazima litokee hapa ni kufufuka kiimani katika Yerusalemu na kujengwa
upya kwa hekalu.

Hivi sasa, mji huo bado unakaliwa na wageni ambao wako hapo. Jambo kuu ambalo litatokea katika taifa la Israei ni lile
linalohusu jinsi kujitokeza kwa wayahudi maalum 144,000 wakati wa dhiki kuu.

Hekalu itajengwa upya.

Danieli 9:27 na 11:31
na Mathayo 24:15
na 2 Thessalonika 2:4
na mwisho Ufunuo 11:1-2

hapa twasoma jinsi vile hekalu itajengwa upya.

Unabii wa mtume Yohana katika Ufunuo 11 uliandikwa baada ya hekalu iliyotangulia kuharibiwa mwaka wa 70 AD.

Kwa hivyo yale mtume Yohana anayoyataja hapa katika Ufunuo lazima yawe ni yale yatakayotokea baadaye.

Waliobaki katika taifa la Israeli baada ya dhiki kuu watafufuka kiroho pale mwokozi wetu Yesu Kristo atakapojitokeza kwenye mlima wa mizeituni atakaporudi mara ya pili:

"Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa mizeituni,
unaolekea Yerusalemu upande wa Mashariki,
nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake,

upande wa mashariki na upande wa magharibi;
litakuwako huko bonde kubwa sana;
na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini"
(Zek.14:4).

Watu wengi wanangoja siku hii kwa hamu.

Wakati mmoja aliyekuwa meya wa Yerusalemu Teddy Kollek alisema kwamba ni yeye aliyekuwa na kazi kubwa
sana ya umeya duniani,

yaani kuandaa mji huo kumpokea Masihi. 

Itaendeleaaa..........

Ni mimi ndugu yako mpenzi

        Ev. Elimeleck S Ndashikiwe.

Tel +255715445846
       +255767445846

0 comments:

Post a Comment