Pages

Subscribe:

Saturday, 14 February 2026

SILAHA KAMILI ZA MUNGU

🔥 SILAHA ZA KIROHO ZA KUSHINDA NGUVU ZA GIZA

Na: Ev ELIMELECK S NDASHIKIWE 

UTANGULIZI
Wapendwa, vita tuliyonayo si ya damu na nyama! Adui yetu si jirani, si binadamu — bali ni falme za giza. 
      Kama inavyoandikwa katika Biblia (WAEFESO 6:12), tunashindana na falme na mamlaka za giza.


Lakini nina habari njema leo 

    HATUJAPEWA ROHO YA WOGA! Tumepewa mamlaka na silaha za ushindi!

1️⃣ MKANDA WA KWELI – SIMAMA KATIKA UKWELI
Uongo ni silaha ya shetani.
      Lakini ukweli ni silaha ya Mungu.
Yesu alisema, “Mtaijua kweli, nayo kweli itawaweka huru.”

Ukiishi katika ukweli:
Huna hofu
Huna mashaka
Adui hana pa kukushika

🔥 Sema: Ninasimama katika ukweli wa Mungu!

2️⃣ DIRII YA HAKI – LINDA MOYO WAKO

Dhambi humpa adui nafasi. Lakini haki hufunga milango ya giza.
Unapotembea katika utakatifu, unavaa ulinzi wa mbinguni.
🔥 Sema: Ninavaa dirii ya haki leo!

3️⃣ NGAO YA IMANI – ZIMA MISHARE YA MOTO

Mashambulizi ya adui huja kwa njia ya:
Hofu
Mashaka
Maneno mabaya
Ndoto za kutisha

Lakini imani inazima mishale yote ya moto!
Kama inavyoandikwa katika Waefeso 6:16 — ichukueni ngao ya imani.
🔥 Sema: Imani yangu haiwezi kuzimwa!

4️⃣ UPANGA WA ROHO – NENO LA MUNGU

Hii ndiyo silaha ya kushambulia!

Yesu alipokuwa akijaribiwa jangwani, alishinda kwa kusema, “Imeandikwa!”
Neno la Mungu linavunja laana, linaangusha ngome, na kufungua vifungo!
 2 WAKORINTHO 10:4, silaha za vita vyetu zina nguvu katika Mungu kuangusha ngome.

🔥 Tangazia hali yako: IMEANDIKWA!

5️⃣ MAOMBI – NGUVU YA SIRI

Hakuna ushindi bila maombi.
Maombi ni mawasiliano na mbingu.
Maombi hubadilisha hali.
Maombi huleta moto wa Roho.

🔥 Omba bila kukoma!

HITIMISHO: USHINDI NI WAKO!
        Wapendwa, huna haja ya kuogopa wachawi wala kuzimu.
Yesu tayari alishinda msalabani!

Simama. Vaa silaha. Tumia mamlaka yako.
🔥 Sema kwa sauti kubwa:
Mimi ni mshindi!
Nimeshinda kwa damu ya Yesu!
Hakuna nguvu ya giza itakayenishinda!

Nipigie Kwa

+255 698 52 50 10

Wednesday, 11 June 2025

UHUSIANO KATI YA MAOMBI NA SADAKA

UKWELI KUHUSU MAOMBI NA SADAKA


Ndugu Yangu Ukweli Kwamba hakuna aliyefanikiwa ambaye haombi wala hatoi Sadaka

Kila aliyefanikiwa Ujue anaomba either MUNGU au Miungu lakini anaomba na anatoa sana Sadaka Kwa MUNGU au miungu

Ni kwa Sababu mwanadamu anayeweza Kufanikiwa binafsi bila msaada wa nguvu za rohoni kutoka kwa MUNGU au Miungu

Na njia mojawapo Ya Kujiconect na msaada wa nguvu ya roho ni Kupitia Maombi na Sadaka

HIVYO KAMA UNATAKA KUFANIKIWA, KAMA UNATAKA KUSTAWI, KAMA UNATAKA KUWA SALAMA BASI MOJAWAPO YA GHARAMA KUBWA UNAYOPASWA KUILIPA NI MAOMBI NA UTOAJI BILA KUJIHURUMIA KATIKA UTOAJI WA SADAKA 
Unapaswa Kuyafanya MAOMBI Na, Sadaka Kuwa Kipaumbele kwenye Maisha Yako

Unapaswa Kuwa na Nidhamu Kubwa Sana Kwenye MAOMBI NA UTOAJI SADAKA

Unapaswa Kuhakikisha Maombi Na Utoaji SADAKA Yanakuwa Maisha Yako

Unapaswa Kuhakikisha HAKUNA SIKU INAPITA BILA KUKAA KWENYE MAOMBI

Wala Hakuna Fedha inayopita mikononi mwako pasipo kuitolea Sadaka

*Unapaswa KUJITOA, KUJIDHABIHU MNO KWENYE MAOMBI KULIKO KAWAIDA MAANA KIWANGO UNACHOOMBA NDICHO KINAAMUA KIWANGO CHA UTENDAJI WA MUNGU KWENYE MAISHA YAKO*

UNAPASWA KUJIDHABIHU MNO KWENYE UTOAJI SADAKA MAANA KIWANGO CHAKO CHA UTOAJI PIA KINAAMUA KIWANGO CHA MUNGU KUKUAMINI KWENYE MAMBO MAKUBWAA

Matendo ya Mitume 10:4
[4]Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana? Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu. 

👆👆Kornelio hakuwa ameokoka hivyo hakuwa na haki Ya MUNGU kumtokea Kupitia Malaika lakini kwa sababu aliziishi kanuni za MUNGU za KUDUMU KATIKA KUOMBA NA KUTOA SADAKA, MUNGU alimtokea Kupitia Malaika na kumpa maelekezo

Usiishie tu Kuomba halafu KUTOA uko nyuma, wala usitoe halafu Kuomba huombi fanya vyote ili upate Matokeo Kwa haraka



Barikiwa

ELIMELECK NDASHIKIWE 
+255 698 525 010

Tuesday, 11 February 2025

NGUVU YA SADAKA

WHAT IS SACRIFICIAL GIVING ? 
         Sacrificial giving is an unusual, uncommon, excellent, outstanding, painful and extra ordinary giving that cost you much in order to attract the attention of God towards your life.

Sacrificial giving is a demand from a higher love to know your level of live, worship, commitment and service for him. Genesis 22:28

sacrificial giving is what you do to destroy the deverstating plans against your life and future. I Chronicles 21:22-25

       Sacrificial giving is a new foundation that we lead to build a strong or fresh future for your destiny. Hebrews 13:16. Living a good life of sacrifices, God is well pleased.

Sacrificial giving is the act of love to show God how important he his in your life.

         Sacrificial giving is a painful act towards a personality you reference or respect much t show your respect to him.

Sacrificial giving is displeasing yourself to please God.

NIDHAMU NI KITU MUHIMU SANA KWA MKRISTO



Kama ambavyo tumekuwa tukijifunza Nguvu Ya Nidhamu binafsi Katika nafasi Ya Mafanikio

Sasa lazima tutambue Kuwa tunaishi Kwenye ulimwengu,Dunia hii 

      Kama tunaishi Kwenye ulimwengu huu Lazima tutakutana na Changamoto za hapa na Pale, lazima tutakutana na Vita , lazima tutakutana na Upinzani Kwenye Mambo mbalimbali, lazima tutakutana na vipindi vigumu Kwenye Maisha

       Maadam tunaishi Kwenye Dunia hii lazima tutakutana na hayo mambo hatuwezi Kuyakwepa Kamwe Wala Kuyakimbia 

       Sasa Moja Kati Ya SILAHA KUBWA itakayokusaidia Kuishi Maisha Ya Ushindi katika Dunia hii Katikati Ya Vita Zote, Katikati Ya Mazingira yoyote, Katikati Ya Changamoto Zozote, Katikati Ya Magumu Yoyote

SILAHA HIYO NI KUISHI MAISHA YA NIDHAMU BINAFSI KATIKA MAMBO YA MUNGU KWA MWENDELEZO

Ukifanikiwa Kuishi Maisha Ya Nidhamu Binafsi Kwenye Mambo Ya MUNGU Kwa Mwendelezo utafanikiwa Kuishi Maisha Ya Ushindi Katika Dunia hii

Hiyo ndiyo Siri iliyosababisha Watu Wengi sana Kuishi Maisha Ya Ushindi katika Dunia hii,hii ndiyo Siri inayotufanya Watu Wengi sana tuishi Maisha Ya Ushindi katika Dunia hii

Pamoja na Changamoto Zote tunazokutana nazo lakini tunashinda,Pamoja na Vita Zote tunazokutana nazo lakini tunashinda, Pamoja na Magumu Yote tunayokutana nayo lakini tunashinda, Pamoja na Upinzani tunaokutana nao kwenye huduma, kwenye Ndoa , kwenye uchumi lakini tunashinda na zaidi Ya Kushinda

MAISHA YA NIDHAMU BINAFSI KWA MWENDELEZO KATIKA MAOMBI KUHAKIKISHA KILA SIKU UNAOMBA, USOMAJI WA NENO, UTOAJI BILA KUJIHURUMIA HURUMIA, MAISHA YA MIFUNGO, MAISHA YA IBADA, NIDHAMU BINAFSI KWENYE KUISHI MAISHA MATAKATIFU NDIYO SIRI YA KUKUWEZESHA KUISHI MAISHA YA USHINDI KATIKA DUNIA HII 

NINAO Ushahidi wa hili ninalokuambia 

Kwa SABABU UNAPOISHI MAISHA YA NIDHAMU BINAFSI KWA MWENDELEZO KATIKA MAMBO HAYO YANASABABISHA UWEPO WA MUNGU UNAKUWA NAWE, YANASABABISHA MKONO WA MUNGU KUTENDA KAZI KWAKO, YANASABABISHA KUWA KARIBU NA BWANA ALIYE NGUZO ,ALIYE NGAO ,ALIYE MSAADA WA KWELI NA HIVYO KABLA LOLOTE HALIJATOKEA BWANA ANAKUPA TAARIFA

Tunajifunza hili Kupitia mfano huu Wa Daniel
👇👇👇👇

Baada Ya Daniel Kuwekwa Juu Ya Viongozi wengine kwenye nchi Ya Babeli Na Wale viongozi walio chini Yake Wakapanga njama za kusababisha Daniel anaondolewa kwenye ile nafasi

Danieli 6:2
[2]na juu yao akaweka wakubwa watatu, na Danieli alikuwa mmoja wao; ili maliwali hawa watoe hesabu kwao, mfalme asipate hasara. 

Na ikawekwa Sheria Mtu yeyote asiombe Kwa mungu awaye yeyote Kwa muda Wa Siku 30 na endapo Mtu yeyote atafanya kinyume angetupwa kwenye tundu la SIMBA

Danieli 6:7
[7]Mawaziri wote wa ufalme, na manaibu, na maamiri, na madiwani, na maliwali wamefanya shauri pamoja ili kuweka amri ya kifalme; na kupiga marufuku, ya kwamba mtu ye yote atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme atatupwa katika tundu la simba. 

Na tunaona Daniel akitupwa kwenye tundu la SIMBA baada Ya kukaidi agizo hilo

Danieli 6:16
[16]Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danieli, wakamtupa katika tundu la simba. Mfalme akanena, akamwambia Danieli, Mungu wako unayemtumikia daima, yeye atakuponya.

Tundu hilo la SIMBA ambapo Daniel alitupwa lilikuwa ni mahali ambapo Mtu akitupwa humo hawezi kutoka tena Maisha Yake ndiyo Yalikuwa Yamefikia Mwisho ni lazima tu ataliwa na kugeuzwa kuwa chakula Cha SIMBA

Lakini Safari hii ikawa ni tofauti Kwa Daniel historia mpya ikaandikwa

Lakini Nini Siri Ya Ushindi Wa Daniel 
👇👇👇

Danieli 6:10
[10]Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.

👆👆👆 Hii ndiyo Siri Ya Ushindi Wa Daniel alikuwa akiishi MAISHA YA NIDHAMU BINAFSI KATIKA MAMBO YA MUNGU KWA MWENDELEZO

Alikuwa Kila Siku lazima ahakikishe anaomba mara 3 Kwa Siku bila Kuacha Wala kukatisha Katisha, licha Ya majukumu aliyokuwa nayo lakini alikuwa lazima ahakikishe anaomba mara 3 Kwa Siku

Maisha Ya hayo Ya Nidhamu Binafsi Yalisababisha Uwepo Wa MUNGU Kuwa naye , Yalisababisha BWANA Kuwa karibu naye , Yalisababisha Mkono Wa MUNGU kutenda kazi kwake

Hata alivyotupwa kwenye tundu la SIMBA hawakuweza kumfanya chochote

Unataka Kuishi Maisha Ya Ushindi katika Dunia hii Jifunze Siri hii kubwa

Ishi Maisha Ya Nidhamu Binafsi Kwenye Mambo Ya MUNGU Kwa Mwendelezo

Hakikisha Unakuwa na ratiba zinazoeleweka za Maombi,ratiba zinazoeleweka za Usomaji Wa Neno, ratiba zinazoeleweka za Mifungo, ishi Maisha Ya Utoaji Kwenye Kile ambacho BWANA anapitisha kwenye mikono Yako, ishi Maisha Matakatifu

Ninao Uhakika UTAUONA MKONO WA BWANA Katikati Ya Magumu utakayopitia, UTAUONA MKONO WA BWANA Katikati Ya Vita utakazokutana nazo, UTAUONA MKONO WA BWANA Katikati Ya Upinzani utakaokutana nao kwenye eneo lolote la maisha Yako

BARIKIWA 


Wednesday, 10 April 2024

THE BENEFITS OF SACRIFICIAL GIVING


The benefits of sacrificial giving

Thought it was wise to write briefly on today's sermon.



Text : Mark 12:41-44
      Note. Sacrifice is the foundation of every power. There is no greatness without sacrifice.

*Any giving to God that is not painful, then it is not a sacrifice. II Samuel 24
*sacrificial giving is not giving any amount of money or large amount of money.
*what ever you have that cannot change your situation is SEED. So when you sow, it gives results and have more than(10) ten or it.
*Every desire of a man to be accomplished is by sacrifice.

     WHAT IS SACRIFICIAL GIVING ? 
  1. Sacrificial giving is an unusual, uncommon, excellent, outstanding, painful and extra ordinary giving that cost you much in order to attract the attention of God towards your life.

  2. Sacrificial giving is a demand from a higher love to know your level of live, worship, commitment and service for him. Genesis 22:28

  3. sacrificial giving is what you do to destroy the deverstating plans against your life and future. I Chronicles 21:22-25

  4. sacrificial giving is a new foundation that we lead to build a strong or fresh future for your destiny. Hebrews 13:16. Living a good life of sacrifices, God is well pleased.

  5. Sacrificial giving is the act of love to show God how important he his in your life.

  6. Sacrificial giving is a painful act towards a personality you reference or respect much t show your respect to him.

  7. Sacrificial giving is displeasing yourself to please God.


  BENEFITS OF SACRIFICIAL GIVING  
  1. General blessing: every time you give a Sacrificial blessing, you keep a generational blessing and also the connected.

  2. You a victory your enemies. II kings 3:27

  3. Harvest rejoy

4.Heavenly recognition. Matthew 26:6-13, Mark 12:41-44

  1. Protection and intervention. I chronicles 21:22-26

  2. All round family blessing. Every time you sacrifice, you tell God to step into your family

  3. Devine Providence. This is when you become to relevant to God, the devil can not pull you down. Romans 12

Thanks for being a part taker of his wo

Monday, 29 August 2022

MZEE MITOMINGI

JINA LA KITABU: NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE
MWANDISHI: EDWIN SEMZABA
WACHAPISHAJI: NYAMBARI NYANGWINE PUBLISHERS
MWAKA: 2006

NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE image

UTANGULIZI WA KITABU
Ngoswe penzi kitovu cha uzembe ni tamthiliya maarufu sana ambayo imewahi kuigizwa katika redio Tanzania na katika majukwaa mbalimbali hapa nchini. Ni tamthiliya ambayo imeundwa vyema katika vipengele vya fani na maudhui. Ameteua lugha nzuri na yenye mvuto kwa wasomaji yenye mbinu za kifasihi zilizosheheni, muundo wenye mtiririko mzuri, unaoakisi kuanza kuchipuka kwa matukio mpaka kilele cha matukio. Wahusika wamebeba vyema uhusika wao mfano Ngoswe.
Ameibua dhamira kuhusu mambo yanayoigusa jamii ya leo kama vile uzembe, madhara ya ulevi, uzembe kazini, suala la matabaka kati ya mjini na vijijini. Mtazamo, falsafa na msimamo wake ni kulenga kuibadilisha jamii na kuleta maendeleo.

JINA LA KITABU
Jina la kitabu “Ngoswe penzi kitovu cha uzembe” ni jina ambalo limesawiri vyema yaliyomo ndani ya kitabu hicho, kwani Ngoswe ndio jina la mhusika mkuu anayebeba dhamira kuu ya tamthiliya. Pia penzi limeonekana kuwa ni kitovu cha uzembe kwani ndio yaliyopelekea kuteketezwa kwa karatasi za takwimu za sensa. Hivyo jina la kitabu si tu kwamba limesawiri yaliyomo katika kitabu bali pia katika jamii.
FANI
MTINDO
Mtindo alioutumia mwandishi ni dayalojia au majibizano. Mwandishi amepanga visa na masimulizi kwa kutumia majibizano ya wahusika.
  • Matumizi ya nafsi
Matumizi ya nafsi ya kwanza. Mwandishi ndiye ameyafafanua na kuelezea baadhi ya matukio. Katika karibu kurasa zote mwandishi ameonekana kuwa ndiye msimuliaji wa matukio.
Matumizi ya nafsi ya pili
Hapa watu wawili na zaidi wanajibizana. Tamthilya hii wahusika wanaojibizana kuibua dhamira na migogoro. Kuna majibizano baina ya mzee Mitomingi, Ngoswe na Mazoea nk.unaweza kupata mfano uk. wowote kwani ndio mtindo uliotawala.

MUUNDO
Muundo uliotumika ni muundo wa mojakwamoja au sahili. Kwani ameonesha tangu mwanzo wa mambo mpaka mwisho, anajenga visa vidogo mpaka visa vikuu au kileleni.
Amepanga visa na matukio yake katika maonesho matano. Kila kichwa kina maelezo yaliyojadiliwa katika onesho hilo.

KIJITO
Hapa yanaeleza jinsi mambo yanavyoanza. Jinsi Ngoswe anavyoingia kijijini anavyopokelewa na kuanza kufahamiana na wenyeji wake.

VIJITO
Hapa Ngoswe anaanza kufanya kazi iliyompeleka kijijini na tunaanza kuoneshwa changamoto anazokumbana nazo.

MTO
Ni mwendelezo wa matukio ya mwanzo hapa visa vinazidi kukua.

JITO
Hapa Ngoswe anakumbana na changamoto nyingi zaidi katika kazi yake. Na hapa anazidi kuanguka kwani anajiingiza katika mapenzi na msichana Mazoea, anaendekeza ulevi na kuharibu kazi kabisa.

BAHARINI
Hapa inaoneshwa mwisho wa mambo jinsi yalivyokuwa. Yanaonekana mahojiano baina ya Serikali na Ngoswe na Mitomingi juu ya uzembe uliofanyika wa kupoteza takwimu na hapa ndipo suluhisho linapotolewa juu ya matatizo hayo.

WAHUSIKA
NGOSWE
  • Kijana wa kiume umri kati yamiaka 20-25
  • Ameelimika na amestaarabika
  • Anatumwa na serikali kufanya sensa kijijini
  • Anajihusisha na mapenzi na msichana mazoea
  • Ni mlevi
  • Hana umakini katika kazi
  • Aliharibu kazi ya serikali
  • Hafai kuigwa na jamii
MAZOEA
  • Ni msichana mwenye umri kati ya miaka 18-20
  • Ni binti wa Mzee Ngengemkeni Mitomingi
  • Hana elimu na hajastaarabika
  • Ana nidhamu ya woga
  • Ana tama
  • Hana msimamo alikubali kuchukuliwa na Ngoswe hali akijua alishatolewa mahari
  • Hafai kuigwa na jamii
NGENGEMKENI MITOMINGI.
  • Ni balozi katika kijiji chake
  • Ni baba mzazi wa Mazoea
  • Ameoa ndoa ya mitara, ana wake wawili
  • Hajaelimika
  • Anashikilia mila na desturi za kale
  • Mlevi
  • Mkali sana
  • Anateketeza karatasi za takwimu.
MZEE JIMBI
  • Mwanakijiji
  • Hajaelimika kwani hajui hata umri wake
  • Ni mlevi
  • Ana wake wawili
  • Anashikilia ukale
MAMA MAZOEA
  • Mke mkubwa wa Mitomingi
  • Mama yake Mazoea
  • Mlezi wa familia
  • Hapewi nafasi ya kutoa maamuzi katika familia
MAMA INDA
  • Mke wa pili Mzee Mitomingi
  • Mama yake Huzuni
  • Hapewi nafasi ya kutoa maamuzi
  • Ni mlezi wa familia.

MANDHARI
Mandhari ya tamthiliya hii imechorwa katika mazingira ya kijijini. Mambo yanayoelezwa ni ya kijijini mfano kilimo, hali ya watu kimaisha, huduma duni sana za kijamii kama vile shule, umbali wa makazi toka nyumba moja hadi nyingine. Haya yanatudhihirishia vyema mandhari hiyo ambayo kwayo imeibua dhamira mbalimbali kama vile umaskini, ukosefu wa elimu, huduma duni za afya vijijini, masuala ya imani potofu nk.

MATUMIZI YA LUGHA
Lugha aliyotumia mwandishi ni lugha fasaha na rahisi kueleweka kwa wasomaji. Pia kuna matumizi ya lugha nyingine mfano uk. 1 “bell bottom”
  • Matumizi ya semi.

Methali
Uk.22 “Penye nia pana njia”.
Uk.27 “Waona vyaelea vyaundwa.”

Misemo
Uk.14 “Akuwaniae ujovu haji kweupe”

Nahau
Uk.11 “hebu keti tutupe mawe pangoni” – tule chakula
Uk.7 “mbongo zimelala”- ana maarifa
Uk.14 “pombe na yeye ni pete na chanda”- anapenda pombe sana.

  • Matumizi ya tamathali za semi.
Tafsida
Uk.21 “Wala hajarudi, kama ingekuwa ni kujisaidia si angekuwa amekwishamaliza?”

Tashbiha
Uk.1 “vumbi jekundu kama ugoro wa subiana”
Uk.8 “sarawili yake miguuni kama kengele ya bomani”
Uk.17 “wanaondoka huku wakitazamwa kama vile mizuka”
                             
Sitiari
Uk.7 Mama Mazoea : “kiziwi mkubwa wee!”
Uk.14 “pombe na yeye ni pete na chanda!”
Uk.26. “karatasi? za takwimu? Ndio wanyama gani hao?”

Mubaalagha
Uk.11 Mama Mazoea : “kupeleka chakula ndio umefanya makao!”
Mama mazoea : “Kujibu swali ndio ukachukua mwaka mzima!”

  • Mbinu nyingine za kisanaa

Mdokezo
Uk.22 Mazoea : “sijui….. siwezi….. namuogopa baba”
Uk.16 Ngoswe : “huyo mtoto wenu wa kwanza anaishi hapa au…..”

Takriri
Uk.9 “Mama Masikio! We Mama Masikio!”
Uk.13. “Hodi! Hodi!”
Uk.2 “karibu karibu”

Tashtiti
Uk.5 Ngoswe: “hivyo waitwa nani?”
Mazoea: “mie?”
Uk.22 Ngoswe: “mchumba? Kwani mchumba ni kitu gani?”
Uk.26 Mitomingi: “karatasi? Za takwimu? Ndio wanyama gani hao?
Hapa wahusika waliuliza maswali ambayo majibu yake waliyaelewa ila kutokana na kutaka kudhihirisha hasira, msisitizo nk. Ndio maana wametumia tashtiti.
                   
Onomatopea/tanakali sauti
Uk.7 Kifaruhande anacheka “Ha! ha! ha!
      
  • Ujenzi wa taswira
Mwandishi ametumia taswira ya mto kuelezea visa vyake. Sehemu ya kwanza ni sehemu ya kijito, kijito ni kimto kidigo mwandishi hapa  anaanza kueleza mambo yakiwa machanga kabisa ndio yanaanza.

Sehemu ya pili ni vijito. Huu ni muunganiko wa vijito vidogovidogo hapa mwandishi anaanza kueleza visa  vidogovidogo. Sehemu inayofuata ni sehemu ya Mto. Hii inaashiria mambo yameanza kuwa mazito, visa vinakua zaidi na Ngoswe anazidi kuingia katika changamoto kubwa zaidi.

Pia Jito ni taswira ambayo mwandishi  ameitumia kuashiria hatari zaidi mambo makubwa zaidi na hapa ndipo tunaona Ngoswe anaanguka kabisa katika kazi yake kwani Jito ni lenye maji mengi na yanayoenda kwa kasi hivyo huhitaji umakini mkubwa zaidi.
Mwisho sehemu ya Bahari ambapo hapa ndipo hatima ya mambo inaelezwa Ngoswe anazama na kupotea kabisa! Hafanikiwi kutoa takwimu kwani karatasi zilichomwa moto.

Thursday, 25 August 2022

NGUVU YA AGANO


Alhamisi 25 August 2022

NGUVU YA AGANO 

Na Mwalimu ELIMELECK NDASHIKIWE

        Hakika ni jambo la kushangaza kwani siku chache zilizopita nilikuaidi kukuandikia kitabu hiki cha Nguvu ya Agano kama Mungu atanipa kibali na siku ile alinipa, leo amenitaka kuanza kukumegea baadhi ya vitu vilivyomo kwenye hicho kitabu na nilikuaidia kuwa katika kitabu hiki nitazungumzia kiundani aina yote ya maagano ikiwemo yale ya Mungu na yakipepo.

          Atukuzuzwe Mungu juu mbinguni na duniani ilipo sehemu ya kuweka miguu yake, leo nitakujuza kiundani kuhusu maagano ama Nguvu iliyopo kwenye maagano ambayo tunaingia na Mungu. Pia jambo hili likupe kiu yakuingi agano ama maagano binafsi na Mungu ili kuwa katika uwakika mkubwa wakutembea na Mungu, kwani kama kuna kitu Mungu hukiheshimu ni Agano.


        Agano ni mapatano baina ya pande kuu mbili au zaidi dhidi ya jambo fulani. 

       Katika maagano ama Agano kuna mambo kadha wa kadha kama nilivyokujuza huku nyuma, ikiwemo, Ishara, Mapatano, ama makubaliano, Kiapo cha uamainifu na kadhalika. Huko mbeleni katika kitabu hiki nitakujuza kwa undani zaidi kuhusu mambo hayo.

      Nataka tuione hiyo Nguvu iliyopo katika maagano ya kimungu ikiwa ni baada ya kuiona iliyopo kwenye maagano ya kipepo siku kadhaa zilizopita kwenye makala ya Msaada kwa wanaoota ndoto wakiwa wanakula vyakula.Pamoja na zile za Namna ya kujinasua kwenye vifungo vya pepo mahaba.

         Kumbuka pia Bibilia ni Agano au ni mkusanyiko wa maagano makuu mawili, yaani lile la Kale na Jipya, ndio maana hutaacha kumuona Mungu kama utasoma Bbilia kwa Sura ya Kiagano, na ufahamu ni kati ya Mwanadamu na Mungu. Na Agano ni mapatano. Ukisoma kwa mtazamo huo wa kuona kilichopo ndani yake kuwa ni mapatano baina yako na Mungu hutatoka kama ulivyo mara baada ya kusoma maandiko na hutakubali kusoma kwa sura ya kawaida ama mazoea.



1. AGANO LA IBRAHIMU:
         Kuna Agano Mungu alifunga na Ibrahimu aliye baba yetu wa imani na Agano hili limekuwa na Nguvu kubwa sana  na Nguvu moja wapo ni hii. Tulione hilo Agano, Agano hili limetiwa nguvu katika sura kadha wa kadha za kitabu hiki cha Mwanzo kwa hiyo tutatazama kila kipengele kilichopo miongoni mwa Agano hili kulingana na uhitaji wa hoja nitakayo ijenga katika mada ama pwenti husika,ila nataka kukudokezea kipengele kimoja kabla ya kusonga mbele zaidi.

           Ni Mwanzo 15: 18 
Siku ile Bwana akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati,
19 Mkeni, na Mkenizi, na Mkadmoni,
20 na Mhiti, na Mperizi, na Mrefai,
21 na Mwamori, na Mkanaani, na Mgirgashi, na Myebusi.

    Umeliona hilo jambo hapo? Tutalichambua huko mbeleni.
(a) Lili husika katika kumbariki Kiuzao Ibrahimu, Kikawaida Ibrahimu umri wake wa kupata mtoto ulikuwa umepita, ila kwa sababu ya Agano hili la Mungu kumpa uzao na ambao utakuwa kama Mchanga wa Bahari na kuwa tajiri Mungu alilazimika kutimiza jambo hilo bila kuangalia kikwazo cha Umri wake ama ule wa mkewe.

       Tuone hiyo ahadi ya uzao kiagano, 
Mwanzo 17: 
      Agano langu nitalifanya imara kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako.

     8 Nami nitakupa wewe na uzao wako baada yako nchi hii unayoikaa ugeni, nchi yote ya Kanaani, kuwa milki ya milele; nami nitakuwa Mungu wao.

     9 Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada yako.

     10 Hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa.

Katika hilo hakuna namna Mungu angeweza kuacha kumpa Isaka, maana tayari ameshajifunga na kiapo, na makubaliano yaliyopo kwenye Agano hilo.

      Kumbuka Lengo kuu la kitabu ama mafundisho haya ni kukupa mwanga wa kuyatumia maagano haya yaliyopo kweye bibilia ili kujinasua mahali ulipo ama kunufaika na Baraka zilizomo ndani ya Bibilia maana bibilia ni mkusanyiko wa maagano makuu mawili yaani lile la Kale na Jipya ambalo maandiko huliita kuwa ni bora zaidi.

       Wakati tunasonga mbele  nataka kukupa uwakika wa kwamba Baraka hizi ni matokeo ya Agano hilo, ndiposa Ibrahimu akampata huyo mwana bila kuangalia umri wake ama kigezo chochote kile cha kibaolojia ili na wewe kama mwana wa Agano hili uwe na ujasiri wakumuomba Mungu bila kuangalia kizuizi chochote kile kilichopo mbele yako.


     Tudhibitishe jambo hili kutoka kwenye kinywa cha Mungu mwenyewe, 
Ni Mwanzo 17: 21 
        Bali agano langu nitalifanya imara kwa Isaka, ambaye Sara atakuzalia majira kama haya mwaka ujao.
22 Mungu akaacha kusema naye, akapanda kutoka kwa Ibrahimu.

Hapo Ni Mungu anayanena hayo wala Sio Jirani yake na Mungu.

(b) Lilimpa Baraka za Mali, Kumbuka Agano hufanywa Imara kwa sadaka, maombi na kadhalika, ndio maana wale wanaofanya maagano na mapepo hupaswa kutoa kafara za damu za wanyama, ndege, hata watu. Na kanuni hiyo Shetani ameiiga kwa Mungu.
Mara baada ya Ibrahimu kukubali kumtoa Mwanaye Mungu alinena naye kuhusu kumbariki kiuchumi ikiwa ni sehemu ya kiagano.

      Mwanzo 22: 15 
Malaika wa Bwana akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni

16 akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee,

17 katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao;

18 na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.

Hapo panatajwa kumiliki malango ya Adui, maana yake ni kuwa na uwezo wa ulimwengu wa roho wakuteka na kutaifisha mali ama utajiri wa adui zako kisha kuugeuza kuwa wako, kwa kifupi ni kuwafanya mateka wa uchumi. Tulihakiki jambo hilo kwenye kitabu hiki hapa:
Isaya 60: 11 Malango yako nayo yatakuwa wazi daima; Hayatafungwa mchana wala usiku; Ili watu wapate kukuletea utajiri wa mataifa, Na wafalme wao wakiongozwa pamoja nao.

Pia sentesi inayofunga mazungumzo hayo ipo katika mstari wa 18, hapo kwenye kitabu cha Mwanzo, ambayo inadhiirisha dhairi kuwa Agano hili ndilo lililopenyeza Baraka kwa kila taifa duniani, ndio maana mataifa yakitaka kubarikiwa ni vyema kujiunganisha ama kujiambatanisha kiroho na Taifa la Iziraeli. Nataka kukuonyesha sentensi hiyo; “na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia
Najua unatamani kuendelea nami ila kwa kweli muda sio rafiki yangu, ila kabla sijakutaka tuonane kesho, ambapo nitaendelea na Agano hili kabla ya kuchambua lile la Nuhu, na mengineyo, ninataka kukupa uwakika kwamba wewe ni sehemu ya Agano hili la Ibrahimu ili kukujengea Imani dhabiti itakayokusaidia kupata uwalali wa kuingia kwenye maombi leo ili kudai Baraka zako za kiagano kama mwana wa Mungu.

Kabla ya andiko hilo kumbuka Yesu alikuwa akiwaponya watu wengi ila alitia mkaza sana kwa watu wa Uzao wa Ibrahimu, ndio maana alipomuona yule mama mgonjwa alimuhurumia na kusema kuwa imekuaje hivi kwa mtu wa uzao wa Ibrahmu, alikadhalika kwa mama mkaninayo yule aliyebembeleza na kusema kuwa hata mbwa hula makombo ya bwana zao na kisha kutendewa mujuza. Pale unamuona Yesu akisema kuwa alitumwa kwa ajili ya watu wa Uzao wa Ibrahimu, ukiona Uzao wa Ibrahmu kama wewe uliyepita darasa hili langu picha unayoipata pale ni kwamba hii ilikuwa ni kauli ya KIAGANO.

Maana yake ni kwamba Yesu alipaswa kutilia mkazo kwa watu hawa kwa sababu ya Nguvu ya kiagano. Kwa mantiki hiyo Mungu hapendezwi na mateso ama taabu kwa mtu wa Uzao wa Ibrahimu. Yaani wewe uliyeokoka na mimi pia. Maana wapo wa uzao huo kibaolojia ambao ni Wayahudi na wapo wa Uzao huo ambao ni wale wa Imani yaani waliokoka. Na jambo hili limetiwa muhuri na Mungu mwenyewe kimaandiko.

Kwa ujasiri fungua nami maandiko haya hapa: Ni WAGALATIA 3.29 Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Ibrahimu, na warithi sawasawa na ahadi.
Neno ahadi hapo linawakilisha AGANO, Maana kama umekuwa mwanafunzi wangu Mwaminifu na Makini utakumbuka vipengele vyote tulivyo visoma vimesheheni ahadi za Ibrahimu kubarikiwa.
Tukutane kesho, ila kama huja Okoka fahamu kuwa hutaweza kuridhi Baraka hizi na maombi utakayoomba hayatakuwa na Nguvu ya kiagano. Na kwa aliyeokoka hivi sasa ninamtaka kuingia kwenye hayo maombi ya kiagano ili kufungua milango iliyofungwa nakudai baraka zako za Watoto, Utajiri na kadhalika.

                                         

Hakuna maoni: