Pages

Subscribe:

Sunday, 22 November 2020

NGUVU ILIYOKUWAMO NDANI YA UPENDO KUTUOKOA

MUNGU KWETU SISI NI KIMBILIO NA NGUVU
MSAADA UTAKAOONEKANA TELE NYAKATI ZOTE


Bwana Yesu Kristo asifiwe sana mtumishi wa Mungu,

Hakika ninapokaa na kuutafakari upendo mkuu ambao Mungu ameudhihirisha kwetu, macho yangu ya rohoni yanaona vitu vingi ndani ya huo upendo.

        Ndipo nilipogundua ya kwamba kumbe UPENDO ni kama kifurushi kilochotumika kubebea mahitaji ya wanadamu, au zawadi za watoto wa Mungu zitokazo kwa Mungu mwenyewe!


Ev. Elimeleck S Ndashikiwe



      Ndipo nikagundua ya kuwa ndani ya huo upendo kuna vitu vingi sana, nikaona moyo wa Mungu kwa kanisa, wokovu kwa kanisa, mavazi yatupasayo watoto wake vikiwa ndani ya huo upendo!


YOHANA 3:16

Kwa maana jindi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanae wa pekee ili tumuamini yaani tumpokee,

Tupate uzima wa milele uliokuwa umefichwa ndani ya Upendo!


        Msukumo wa kiMungu kutuhitaji wanadamu ili turudi kwenye njia yake, shabaha yake ilikuwa kwanza atuandalie vijizawadi ambavyo vitatushawishi na kuwa chambo kitupeleka kwenye wokovu!

       Pasipo upendo yawezekana angetumia njia nyingine, lkn aliona kuutumia upendo kama package au kifurushi inafaa! Akatununua kwa damu yake ya thamani ili tumuamini.


   KWA NINI TUMUAMINI?

Ni kwa sababu ulimwengu mzima ulikuwa umeigeukia miungu mingine na kuiamini,

        Mungu akaona kabisa haipendezi, ili atuondoe kwenye mikono ya imani nyingine ni lazima atuletee vizawadi vitakavyotushawishi kuvikimbilia kwake, tukishavikimbilia kwake tupate kumsikiliza,

Na tukishamsikiliza tu Imani yake mpya inaingia ndani yetu kwa upya tena, ndiposa tumuamini kwa kuwa chanzo cha imani ni kusikia, tena kulisikia Neno la Kristo.




      Mwamini leo Yesu Kristo kupotia Neno lake, nawe utapokea wokovu mkuu tuliodhihirishiwa bure kabisa!

Tusonge hapa;

              Zaburi 91

1 Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.

2 Nitasema, Bwana ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini.

3 Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, Na katika tauni iharibuyo.

4 Kwa manyoya yake atakufunika, Chini ya mbawa zake utapata kimbilio; Uaminifu wake ni ngao na kigao.

5 Hutaogopa hofu ya usiku, Wala mshale urukao mchana,

6 Wala tauni ipitayo gizani, Wala uele uharibuo adhuhuri,

7 Ijapo watu elfu waanguka ubavuni pako. Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume! Hata hivyo hautakukaribia wewe.

8 Ila kwa macho yako utatazama, Na kuyaona malipo ya wasio haki.

9 Kwa kuwa Wewe Bwana ndiwe kimbilio langu; Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako.

10 Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.

11 Kwa kuwa atakuagizia malaika zake Wakulinde katika njia zako zote.

12 Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

13 Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.


     Nawapenda sana tena sana, Mungu wa mbinguni akubariki sana wewe uliyejaaliwa kuusoma ujumbe huu!


    Na kama una maoni au swali lolote niulize kwa namba

+255 689 240 840


Inapatikana pia kwa njia ya WhatsApp.

Friday, 6 September 2019

KANUNI ZA KIROHO By Ev. Elimeleck Ndashikiwe

    Kila jambo maishani lina kanuni zake.
Kadhalika maisha ya kiroho yana kanuni zake za jinsi ya kushirikiana na Mungu.

     1. MWENYEZI MUNGU ANAKUPENDA, NAYE ANATAKA KUKUPANGIA MPANGO WA AJABU KWA MAISHA YAKO.

       UPENDO WA MUNGU
  Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
       Yohana 3:16

MPANGO WA MUNGU KWAKO
      Mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.
Yohana 10:10

      Je, kwa nini watu wengi hawana uzima huo? Ni kwa sababu . . .

      2. MWANADAMU NI MWENYE DHAMBI.
       Dhambi zake zimemtenga na Mungu.Kwa hiyo hajui upendo na mpango wa Mungu kwa maisha yake.

      MWANADAMU NI MWENYE DHAMBI
Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
        Warumi 3:23

    Mungu alimwumba mwanadamu kwa kusudi la kushirikiana naye, lakini mwanadamu alikwenda kinyume cha mpango wa Mungu.
     Alichagua kumwasi Mungu badala ya kumtii.
  Kumwasi Mungu ni kufanya dhambi.

       Mtu anapoishi kinyume cha mapenzi ya Mungu anaendelea kuishi maisha ya dhambi.

      MWANADAMU AMETENGANA NA MUNGU
    Lakini maovu yenu yamewatenga ninyi na Mungu wenu.
        Isaya 59:2

       Mungu Mtakatifu hana ushirika na dhambi.
       Kati yake na mwanadamu kuna ufa mkubwa wa dhambi.
    Mwanadamu hujaribu kumfikia Mungu kwa nija nyingi:
   dini, matendo mema, sala, n.k., lakini hizi zote hazitoshi.

     Mwanadamu bado ni mwenye dhambi. Kuna njia moja tu ya kushirikiana na Mungu . .

      3. YESU KRISTO NI NJIA YA PEKEE YA KUONDOA DHAMBI.
     Alikufa kwa ajili yetu ili tujue upendo na mpango wa Mungu kwa maisha yetu.
        ALIKUFA ILI ATULETE KWA MUNGU
Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu.
        1 Petro 3:18

      YESU YU HAI
Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yanenavyo maandiko; na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alitufuka siku ya tatu,
     kama yanenavyojil maandiko.
      1 Wakorintho 15:3,4

YESU NDIYE NJIA YA PEKEE
       Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
           Yohana 14:6

      Mwanadamu peke yake hawezi kushirikiana na Mungu. Mungu alimtuma Yesu afe msalabani kwa ajili ya dhambi zetu na tena awe daraja kati yetu na Mungu ili atulete kwa Mungu.

      Sasa kanuni ya nne itakuambia jinsi uwezavyo kumjua maishani mwako . . .

    4. INAKUPASA KUMPOKEA YESU AWE MWOKOZI NA MTAWALA WAKO.
         Ndipo utajua upendo na mpango wa Mungu kwa maisha yako.

   UNAMPOKEA KRISTO KWA IMANI
Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
        Yohana 1:12

   Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.
Waefeso 2:8,9

     INAKUPASA KUMKARIBISHA YESU, MAISHANI MWAKO
     Ndashikiwe
nasimama milangoni, nabisha, mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake . . .

    Kumpokea Yesu Kristo ni:
Kujua wewe ni mwenye dhambi na kugeuka nafsi yako kwa Mungu na kutubu.
      Kumtegemea Mungu kwa kukusamehe kabisa.

   MUNGU WANGU WA MBINGUNI AWABARIKI SANA TENA SANA

   By Ev. Elimeleck Ndashikiwe

    Tel: +255762 680 380

USHINDI

HUWEZI KUWA SHUJAA IKIWA AU USIPOSHINDANA NA UKASHINDA

          Mungu wetu ni mwaminifu wakati wote, anatupatia nguvu ya kushinda na kuweza.

ISAYA 7:14 Yeye ni shujaa anayo mamlaka, uweza na nguvu kutufanikisha ktk hatua zetu zote

MWAMINI YEYE NAWE UTADHIBITIKA, WAHESHIMU NA WATUMISHI WAKE UTAINULIWA.