Pages

Subscribe:

Saturday, 5 September 2015

DHAMBI HUWATENGA WANADAMU NA MUNGU MUUMBA WAO.



BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu.
Karibu tujifunze neno la MUNGU la uzima.
Ni heri wewe kama utalitii Neno la MUNGU.
Leo tunaichambua dhambi na madhara yake.
jambo la kwanza kujua ni kwamba Dhambi Humtenga Mtu Na MUNGU.
Isaya 59:2'' lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na MUNGU wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia. ''.
Ndugu,Ukikubali Kujitenga Na MUNGU Muumbaji Wako Kwa Sababu Ya Dhambi, Chunga Maana Usipotubu Utatengwa Na MUNGU Milele Kwa Wewe Kuwa Jehanamu Huku Wateule Wa KRISTO Wako Mbinguni.
Lakini nafasi ya kutubu bado ipo hivyo itumie. Tunao muda mchache wa kusahihisha njia zetu na kubadilika kabisa kutoka kuitwa waovu na kuanza kuitwa watakatifu kama tu tukiamua kutubu na kuacha dhambi.
1 Yohana 1:9 ''Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. ''
Dhambi ndio kitu cha kwanza ambacho kinakufanya wewe uwe mbali na MUNGU.
dhambi ya Adamu imetuathiri wanadamu wote.
Warumi 5:12 '' Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi; ''
Jambo Lingine la muhimu kujua kuhusu dhambi ni kwamba Roho Itendayo Dhambi Ndio Itakayokufa Maana Yake Ndio Itakayokwenda Jehanamu.
Ezekieli 18:20 '' Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake. ''
Dhambi Haitakiwi Kuwatawala Wanadamu.
Tatizo Kubwa La Wanadamu Ukiwahubiria Waache Dhambi Wanakuona Kama Umeleta Dini Mpya Kumbe Wewe Ndio Umelisimamia Kusudi La MUNGU.
Ona mfano huu ambapo mfalme wa Israel alimwasi MUNGU. Neno la MUNGU lilimfuata likisema
'' Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la BWANA, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.-1 Samweli 15:23 ''
-Dhambi inaweza hata ikasababisha ukaondolewa katika huduma yako.
-Dhambi inaweza ikakuondoa katika mpango wa MUNGU.
-Ukilikataa Neno La BWANA YESU Na Yeye Siku Ile Atakukataa. -Ukiukataa Uzima Usitarajie Kupelekwa Uzimani Kwa Nguvu Bali Utaenda Katika Njia Ya Jehanamu Uliyoichagua.
Jambo jingine muhimu kujua kuhusu dhambi ni kwamba Dhambi Huzaa Mauti Yaani Dhambi Huzaa Jehanamu.
Yakobo 1:15-16 '' Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti. Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike. ''
Ndugu yangu,Kwa Unyenyekevu Mkubwa Nakuonya Uache Dhambi, Nakuomba Umpokee BWANA YESU Ili Upate Uzima. Kumbuka Afuataye Dhambi Hufuata Jehanamu .
Mithali 11:19 '' Haki huelekea uzima; Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe. ''
-Dhambi ni mbaya na dhambi huwapeleka watu jehanamu.
-Kama kuna kitu mwanadamu anatakiwa akiogope basi ni dhambi. na dhambi mbaya zaidi ni kumkataa YESU na kukataa kuongozwa na Biblia.
-Ndugu yangu, nakusihi kuanzia leo kataa dhambi zote na uanze kuishi maisha matakatifu.
Je Nimebakiza Nini Katika Kukuambia?
Nimebakiza Moja, Ishi Maisha Ya Wokovu Matakatifu Siku Zote.
Warumi 6:23 ''Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya MUNGU ni uzima wa milele katika KRISTO YESU BWANA wetu.''
-Ndugu,Naamini umejifunza na utachukua hatua njema ya kumpokea BWANA YESU kama hujaokoka ili awe BWANA na MWOKOZI wako tangu leo na utaanza kuishi maisha matakatifu.
KAMA UNATAKA KUTUBU RUDIA MANENO HAYA KISHA TAFUTA KANISA LA KIROHO UKAJIUNGE NA KUANZA KUISHI MAISHA MATAKATIFU.
''BABA katika jina la YESU KRISTO Niko mbele zako mimi mwenye dhambi, lakini leo nimetambua kosa langu na naomba unisamehe dhambi zangu zote, nisamehe dhambi ninazozikumbuka na pia zile ambazo sizikumbuki. futa jina langu katika kitabu cha hukumu na uliandike jina langu katika kitabu cha uzima. Neno lako katika Warumi sura ya 10 Mstari wa 9 na wa 10 Neno lako linasema ''Kwa sababu, ukimkiri YESU kwa kinywa chako ya kuwa ni BWANA, na kuamini moyoni mwako ya kuwa MUNGU alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu '' . BWANA YESU mimi nimekuamini leo na hivyo naamini sasa napokea wokovu wako na hakika nimeokoka. Kuanzia leo Naufunga ukurasa wa dhambi na ninaufungua ukurasa wa matendo mema na matakatifu. BWANA nipe ROHO wako Mtakatifu ili aniwezeshe kushinda dhambi na anasa zote za dunia. Kuanzia leo mimi nimeokoka na ni mtoto wa MUNGU mwenye haki zote. ninafuta laana zote na kila roho ya shetani inayonifuatilia naiharibu kwa jina la YESU KRISTO kama neno la MUNGU linavyosema katika Yeremia sura ya kwanza mstari wa 10. BWANA YESU nakushukuru sana kwa kuniokoa. Yote haya kwa imani nimepokea na niko tayari sasa kwa ROHO MTAKATIFU kunitumia. Katika jina la YESU KRISTO nimeomba na kupokea . Amen.''
Kama umetubu toba ya kweli hakika wewe kuanzia sasa ni mshindi na ni shujaa. Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine. ulishindwa kumpokea BWANA YESU nafasi yako bado ipo na muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA. MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili

0 comments:

Post a Comment