Pages

Subscribe:

Friday, 25 September 2015

KUREJESHEWA NAFASI YAKO

Mwanzo 25: 21-34………Yakobo akamwambia,kwanza niuzie leo haki yako ya mzaliwa wa kwanza……………..Yakobo akamwambia, uniapie kwanza . Naye akamwapia, akamwuzia Yakobo haki yake ya mzaliwa wa kwanza……………. Tunaona historiya ya watoto wawili ambao walikuwa wanapendwa na wazazi wao lakini mtoto mmoja anapenda kuliko mwingine. Tunaona kuwa tangu kipindi cha ibrahimu alikuwa hana mtoto na alipokuja kupata mtoto alikuwa mbarikiwa naye alikuwa ndiye Isaka,naye Isaka anapata mke naye anakuwa tasa kwa muda mrefu alipokuja kupata watoto wawili mapacha Mungu akamwambia una mataifa mawili ndani yako. Mungu aliona wale watoto wawili kuwa mataifa mawili makubwa,taifa moja litamtumikia mwingine naye alikuwa akiimanisha kuwa taifa moja litakuwa hodari na mkubwa atamtumikia mdogo. Mwanzo 27:1-40 Tunaona rebeka anamwambia mwanae mdogo achukue Baraka ya kaka yake na mama anakubari kuchukua laana naye akamchukulia mavazi mazuri ya esau naye yakobo akaenda akachukua baraka ya Esau. Isaka alimpenda Esau kwa sababu alikuwa anakula mawindo yake lakini biblia haijatuambia Rebeka alimpenda Yakobo,huu sio upendo mzuri maana anakula mawindo yake lakini wakati wa baraka alifukuziwa mbali lakini rebeka alimpenda yakobo basi hatuoni alimpendea kwa kitu gani. Esau alikuwa ni mtu wa nyikani na Yakobo alikuwa mtu wa shambani ,mtu wa mtulivu na Isaka alimwamini Esau kwa mapishi kwa namna haipendayo kuliko Rebeka ndio mana alikuwa anapenda chakula Esau naye rebeka alimpenda yakobo kwakuwa esau alichukua nafasi yake ya mapishi. Rebeka aliyashikilia yale maneno ambayo aliambiwa kuwa ndani ya tumbo lako kuna mataifa mawili na mkubwa atamtumikia mdogo. Yakobo alikuwa mkulima na Esau alikuwa mwindaji,yakobo alikuwa hali mbegu lakini esau alikuwa anakula mbegu kwanini maana alikuwa anawinda mawindo na lazima amjerui na kumchinja kulekule porini na kuja na nyama nyumbani ili wale. Leo hii wapo watu wengi wanakula mbegu na wanataka Mungu awabariki,Mungu hawezi kukubariki kwa namna hiyo kama unakula mpaka zaka na dhabihu. Esau aliuza haki yake ya mzaliwa wa kwanza kwaajili ya dengu la siku moja naye akuzingatia baraka ya mzaliwa wa kwanza Kuna wakati watu wanauza Baraka za mzaliwa wa kwanza kwa shetani wakizani kuwa ndio wanaingia kwenye mafanikio uku wakiona kuwa yale waliyatoa kuwa hayana maana sana.

Ni mimi rafiki yako
Ev. ELIMELECK S NDASHIKIWE
elimelck@gmail.com
+255767445846
+255715445846

0 comments:

Post a Comment