![]() |
BWANA YESU asifiwe ndugu yangu.
Ni mara nyingi sana huwa namshukuru MUNGU
ninapoona maelfu ya watu wamehudhuria mbele
ya MUNGU kujifunza neno la MUNGU, Kupokea
uzima wa BWANA YESU , Kumpa maisha yao
BWANA YESU.
Watumishi wa MUNGU hujitoa sana ili tu injili
imfikie kila mtu. Kuna Mchungaji mmoja rafiki
yangu alifunga siku 11 bila kula wa kunywa
chochote ili MUNGU aguse wanadamu ambao
watakuja katika mkutano wa siku 3 wa neno la
MUNGU ambapo mchungaji huyo alikuwa ni
mfundishani. Watu waliokoka na wengi
walifunguliwa, hakika injili inasonga mbele.
Watumishi wa MUNGU wengi hujitoa miili yao
dhabihu kama neno linavyoaagiza ili tu wewe
uokoke.
Warumi 12:1-2 ( Basi, ndugu zangu, nawasihi,
kwa huruma zake MUNGU, itoeni miili yenu iwe
dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza
MUNGU, ndiyo ibada yenu yenye maana. Wala
msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe
kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua
hakika mapenzi ya MUNGU
Wengine hawakulala usingizi ili wewe na mimi
tuupate uzima wa kweli ulio katika KRISTO
YESU.
Yawezekana ulihudhuria mara moja tu mkutano
wa injili kwa lengo la kuponywa ugonjwa wako,
na MUNGU siku hiyo hakukuponya kwa sababu
alikujua unataka kupona tu harafu uondoke na
kwenda kuwasimanga wahubiri.
Yawezekana ulihudhuria mikutano ya injili lakini
umerudi nyuma je kwa sasa huihitaji tena
mbingu?
Yawezekana ulienda kushangaa watu tu.
Ndugu yangu penda mahubiri na penda uzima wa
milele, na kama utapenda uzima wa milele
utakuwa unampenda YESU KRISTO maana uzima
wa milele hauko kwingine nje na yeye. Na siku
zote BWANA anawatuma wahubiri hao
unaowaona ili wewe umruhusu yeye YESU
kutawala maisha yako.
Ni wakati wa kumpa YESU maisha yako maana
kesho huijui itakuwaje.
Kuna watumishi wa MUNGU wameonekana kama
vichaa mbele ya watu ambao ufahamu wao
umetekwa na shetani lakini hawakukata tamaa,
lengo na nia ya mioyo yao ni watu wampokee
BWANA YESU kama BWANA na MWOKOZI wa
maisha yao kama neno la MUNGU linavyosema
''Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa
kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale
waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu,
wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa
mapenzi ya mtu, bali kwa MUNGU-Yohana
1:12-13''.
Ndugu yangu yawezekana hujawahi kuona
umuhimu wa kuhudhuria mikutano ya injili,
yawezekana ukiwaona wahubiri unawaona tu
kama watu waliokosa kazi, yawezekana mahubiri
yao unayaona kama kelele tu lakini napenda
kukutaarifu kuwa mahubiri yote ambao
utayasikia iwe ni redioni, sokoni au popote ni
MUNGU anakuhitaji wewe ili tu usiende motoni.
Maelfu ya watu wanaokoka lakini yawezekana
wewe haumo kwenye orodha hiyo, unadhani ni
kwanini haumo?
Wengi wanakimbilia uzima wewe uko wapi?
Wengi wanamhitaji YESU usiku na mchana je
wewe uko wapi?
Wengi wanaokoka, je wewe uko wapi?
Wengi wanatamani mahubiri kila siku, wewe je?
Wengi majina yao yanaandikwa kwenye kitabu
cha uzima, wewe je?
Nakushauri kumpokea BWANA YESU leo na
utaona mabadiliko makuu sana.
yawezekana
wewe hauko katika orodha hiyo ya wateule wa
MUNGU kwa sababu tu hukuhudhuria mahubiri. Naomba ujue kwamba muujiza mkubwa kuliko yote ni kumpokea
BWANA YESU kama BWANA na MWOKOZI wa
maisha yako. wewe yawezekana huhitaji kuhudhuria
katika ibaada, unadhani ni kawnini? je
huhitaji mbingu? kundi kubwa LA watu
wanamhitaji YESU lakini wewe haumo, je uko
wapi?
watu
wengi tu wanaokoka lakini yawezekana wewe
haumo katika wale wanaompokea BWANA YESU,
unadhani ni kwanini?. watu wengi
wanafunguliwa na kuokoka lakini yawezekana
wewe haumo kwenye kundi la wanaompokea
YESU, unadhani ni kwanini/ je uko wapi? je
huitaki mbingu leo?
Maelfu ya watu wanaokoka, je
wewe uko wapi? . kundi kubwa LA watub
wanamhitaji BWANA YESU je wewe uko wapi/ je
leo huitaki mbingu?
watu wanatoka mbele ili kumpokea BWANA
YESU kama BWANA na MWOKOZI wa maisha
yao. Yawezekana wewe haupo kwa sababu
hukuhudhuria, je utampokea YESU lini? au je leo
hutaki mbingu?. umealikwa mara ngapi
kuhudhuria ibada, semina au mikutano ya injili
lakini hukuona umuhimu wa MUNGU anayetaka
kukuponya na kukuokoa?
maelfu ya watu
wanampokea YESU lakini yawezekana wewe
haumo kwa sababu ulikataa kuhudhuria.
BWANA YESU amenituma kwa ndugu zangu wote na marafiki.
Mwenye sikio LA kusikia na asikie Leo na kuchukua hatua.
Jehanamu inawangoja watenda dhambi lakini ashukuriwe MUNGU maana mbingu inawasubiri watakatifu wa MUNGU.
Kwa leo naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi
tutajifunza tena siku nyingine.na kama
hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea
ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika
jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza
kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani.
ROHO aliyenipa ujumbe huu ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee
motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO
BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
0714252292
MUNGU akubariki sana uliyesoma
somo hili.
0 comments:
Post a Comment