Pages

Subscribe:

Saturday, 5 September 2015

DHAMBI HUWATENGA WANADAMU NA MUNGU MUUMBA WAO.



BWANA YESU atukuzwe ndugu yangu.
Karibu tujifunze neno la MUNGU la uzima.
Ni heri wewe kama utalitii Neno la MUNGU.
Leo tunaichambua dhambi na madhara yake.
jambo la kwanza kujua ni kwamba Dhambi Humtenga Mtu Na MUNGU.
Isaya 59:2'' lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na MUNGU wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia. ''.
Ndugu,Ukikubali Kujitenga Na MUNGU Muumbaji Wako Kwa Sababu Ya Dhambi, Chunga Maana Usipotubu Utatengwa Na MUNGU Milele Kwa Wewe Kuwa Jehanamu Huku Wateule Wa KRISTO Wako Mbinguni.
Lakini nafasi ya kutubu bado ipo hivyo itumie. Tunao muda mchache wa kusahihisha njia zetu na kubadilika kabisa kutoka kuitwa waovu na kuanza kuitwa watakatifu kama tu tukiamua kutubu na kuacha dhambi.
1 Yohana 1:9 ''Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. ''
Dhambi ndio kitu cha kwanza ambacho kinakufanya wewe uwe mbali na MUNGU.
dhambi ya Adamu imetuathiri wanadamu wote.
Warumi 5:12 '' Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi; ''
Jambo Lingine la muhimu kujua kuhusu dhambi ni kwamba Roho Itendayo Dhambi Ndio Itakayokufa Maana Yake Ndio Itakayokwenda Jehanamu.
Ezekieli 18:20 '' Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake. ''
Dhambi Haitakiwi Kuwatawala Wanadamu.
Tatizo Kubwa La Wanadamu Ukiwahubiria Waache Dhambi Wanakuona Kama Umeleta Dini Mpya Kumbe Wewe Ndio Umelisimamia Kusudi La MUNGU.
Ona mfano huu ambapo mfalme wa Israel alimwasi MUNGU. Neno la MUNGU lilimfuata likisema
'' Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la BWANA, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.-1 Samweli 15:23 ''
-Dhambi inaweza hata ikasababisha ukaondolewa katika huduma yako.
-Dhambi inaweza ikakuondoa katika mpango wa MUNGU.
-Ukilikataa Neno La BWANA YESU Na Yeye Siku Ile Atakukataa. -Ukiukataa Uzima Usitarajie Kupelekwa Uzimani Kwa Nguvu Bali Utaenda Katika Njia Ya Jehanamu Uliyoichagua.
Jambo jingine muhimu kujua kuhusu dhambi ni kwamba Dhambi Huzaa Mauti Yaani Dhambi Huzaa Jehanamu.
Yakobo 1:15-16 '' Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti. Ndugu zangu wapenzi, msidanganyike. ''
Ndugu yangu,Kwa Unyenyekevu Mkubwa Nakuonya Uache Dhambi, Nakuomba Umpokee BWANA YESU Ili Upate Uzima. Kumbuka Afuataye Dhambi Hufuata Jehanamu .
Mithali 11:19 '' Haki huelekea uzima; Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe. ''
-Dhambi ni mbaya na dhambi huwapeleka watu jehanamu.
-Kama kuna kitu mwanadamu anatakiwa akiogope basi ni dhambi. na dhambi mbaya zaidi ni kumkataa YESU na kukataa kuongozwa na Biblia.
-Ndugu yangu, nakusihi kuanzia leo kataa dhambi zote na uanze kuishi maisha matakatifu.
Je Nimebakiza Nini Katika Kukuambia?
Nimebakiza Moja, Ishi Maisha Ya Wokovu Matakatifu Siku Zote.
Warumi 6:23 ''Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya MUNGU ni uzima wa milele katika KRISTO YESU BWANA wetu.''
-Ndugu,Naamini umejifunza na utachukua hatua njema ya kumpokea BWANA YESU kama hujaokoka ili awe BWANA na MWOKOZI wako tangu leo na utaanza kuishi maisha matakatifu.
KAMA UNATAKA KUTUBU RUDIA MANENO HAYA KISHA TAFUTA KANISA LA KIROHO UKAJIUNGE NA KUANZA KUISHI MAISHA MATAKATIFU.
''BABA katika jina la YESU KRISTO Niko mbele zako mimi mwenye dhambi, lakini leo nimetambua kosa langu na naomba unisamehe dhambi zangu zote, nisamehe dhambi ninazozikumbuka na pia zile ambazo sizikumbuki. futa jina langu katika kitabu cha hukumu na uliandike jina langu katika kitabu cha uzima. Neno lako katika Warumi sura ya 10 Mstari wa 9 na wa 10 Neno lako linasema ''Kwa sababu, ukimkiri YESU kwa kinywa chako ya kuwa ni BWANA, na kuamini moyoni mwako ya kuwa MUNGU alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu '' . BWANA YESU mimi nimekuamini leo na hivyo naamini sasa napokea wokovu wako na hakika nimeokoka. Kuanzia leo Naufunga ukurasa wa dhambi na ninaufungua ukurasa wa matendo mema na matakatifu. BWANA nipe ROHO wako Mtakatifu ili aniwezeshe kushinda dhambi na anasa zote za dunia. Kuanzia leo mimi nimeokoka na ni mtoto wa MUNGU mwenye haki zote. ninafuta laana zote na kila roho ya shetani inayonifuatilia naiharibu kwa jina la YESU KRISTO kama neno la MUNGU linavyosema katika Yeremia sura ya kwanza mstari wa 10. BWANA YESU nakushukuru sana kwa kuniokoa. Yote haya kwa imani nimepokea na niko tayari sasa kwa ROHO MTAKATIFU kunitumia. Katika jina la YESU KRISTO nimeomba na kupokea . Amen.''
Kama umetubu toba ya kweli hakika wewe kuanzia sasa ni mshindi na ni shujaa. Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine. ulishindwa kumpokea BWANA YESU nafasi yako bado ipo na muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA. MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili

KATIKA SAA USIYODHANI, BWANA YESU YUAJA.

Na Peter M Mabula

BWANA YESU asifiwe.
Karibu tujifunze neno la MUNGU.
''kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari
kwa kuwa katika saa msiyodhani MWANA WA
ADAMU yuaja {Mathayo 24:44}
Ndugu Zangu,
Siku Ya BWANA I Karibu.
Siku Hiyo Hakutakuwa Na Mwanadamu Wa Kutoa
Udhuru, Hakutakuwa Na Wa Kujitetea "Kwa
Sababu Mambo Yasiyoonekana Na Kufahamika
Kwa Kazi Zake; Yaani, Uweza Wake Wa Milele
Na Uungu Wake; Hata Wasiwe Na Udhuru-
Warumi 1:20 .
Ndugu Utakaa Wapi Katika Maisha Yako Ya
Milele? .
Biblia Inasema
"Mwenye Busara Huyaona Mabaya Na Kujificha;
Bali Wajinga Huendelea Mbele Wakaumia-
Mithali 22:3" .
-Ndugu Yangu Je Wewe Ni Mwenye Busara Au
Mjinga?
Wajinga Wataumia Na Wenye Busara
Watajificha.
-Ndugu Zangu, Siku Ile Pa Kujificha Ni Sehemu
Moja Tu Yaani Kwa KRISTO.
-Ndugu, Nakuuliza Tena Je Wewe Ni Mwenye
Busara Au Mjinga? Hilo Unalijua Wewe Moyoni
Mwako Ila Kama Unataka Kuwa Mwenye Busara
"Mwamini BWANA YESU KRISTO, Nawe
Utaokoka-Matendo 16:31" .
Kama Unautaka Kweli Uzima Wa Milele
KUOKOKA NI LAZIMA. -Kukataa WOKOVU Wa
BWANA YESU Ni Kuukataa Uzima Wa Milele.
- Ndugu Amua Vyema Leo Na Utapata Raha
Nafsini Mwako. YESU Anakuita Leo, Itika Ndugu
Na Mpokee Awe BWANA Na Mwokozi Wa Maisha
Yako.
Dunia nzima wanaungojea ujio wa BWANA YESU,
Na katika saa usiyodhani atakuja, mtii MUNGU
na ishi kama neno la MUNGU linavyokuamuru.
Usijitenge na wokovu wa BWANA YESU maana
katika saa usiyodhani kuna kuondoka. na makazi
kama hujaokoka yatakuwa kuzimu ambapo
haitakiwi mtakatifu yeyote afike huko.
-Kama YESU Atakukwaza Kwa Jambo Lolote
Tambua Kwamba Wewe huuhitaji uzima wa
milele. Yeye anasema
'' Naye heri mtu ye yote asiyechukizwa nami.-
Luka 7:23 ''
-Ukiwa kwa MUNGU unakuwa hauko kwa
shetani.
Ukiwa nje ya MUNGU, moja kwa moja unakuwa
uko kwa shetani. Hakuna sehemu ya kati!
Na BWANA hawataki wote ambao wanasitasita.
Ufunuo 3:15 {Nayajua matendo yako ya kuwa hu
baridi wala hu moto ingekua heri kama ungekua
baridi au moto] -Tunapomchagua MUNGU
tuachane na ya shetani yote sio kwa MUNGU
50% na shetani 50%,
MUNGU BABA atuwezeshe tuchague YESU
KRISTO 100%
Ndugu, kuna kuitazamia hukumu mbaya kama
hatutautambua wakati huu kwamba ni wakati wa
kutubu na kuishi maisha matakatifu.
Kama unapanga kutubu baadae je unauhakika
hiyo baadae yako utakuwa hai?
Wengi walipanga kutubu wakiwa wazee lakini
hata uzeeni hawakufika na kujikuta wako
matesoni kuzimu.
Waebrania 10:26-27 '' Maana, kama tukifanya
dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile
kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi;
bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na
ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.
''
Ndugu zangu, huu sio wakati wa kufurahia
dhambi, kama kuna dhambi ambayo unadhani
huwezi kuiacha nakuomba uende na kumweleza
mchungaji wako naye atakuombea. pia okoka na
kuomba maombi ya ushindi kupitia jina la YESU
KRISTO. Damu ya YESU ina mamlaka ya
kukuweka huru mbali na dhambi zilizokutesa
miaka mingi.
-Damu ya YESU inauwezo wa kuvunja
minyororo yote ya shetani iliyokua imekufunga
kama roho ya pombe, pepo la ngono,uongo,wizi
na chochote cha shetani ambacho ulidhani
haiwezekani wewe kukiacha kitu hicho, muhimu
ni kumpa YESU maisha yako ili uwe huru . -
mfanye BWANA YESU kuwa namba moja
maishani mwako ili uishi mbali na kuonewa na
nguvu za giza pia baada ya ulimwengu huu
upate uzima wa milele.
-Mfanye YESU kuwa rafiki yako wa karibu zaidi.
-kwa sababu YESU ndie rafiki yako wa karibu
zaidi usiache kumshirikisha chochote
kinachokusibu kwani yeye ni msaada wa karibu
sana. BWANA YESU anasema
Yohana 14:13-15 ''Nanyi mkiomba lo lote kwa
jina langu, hilo nitalifanya, ili BABA atukuzwe
ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa
jina langu, nitalifanya. Mkinipenda, mtazishika
amri zangu. ''
-shetani asikuteke ndugu ukashindwa kwenda
kanisani bali mshinde na kumwaibisha kwa
kwenda kanisani ukiwa wa kwanza na tena tenda
mema sawasawa na neno la MUNGU.
Hakuna ambacho BWANA YESU hawezi
kukitengeneza na kikawa sawa. Sauli alikuwa
Jambazi muuaji aliyeshindikana lakini
alipokutana na BWANA YESU akageuka muhubiri
wa neno la MUNGU kwa mataifa.
-Kuna siku usiyoidhani huko mbeleni utaondoka,
je ukiondoka utaenda mbinguni? maana
mbinguni wanaingia watakatifu tu waliomtii
KRISTO enzi za uhai wao. je utakuwa mmoja
wao?
-Zishinde dhambi kwa kumwita BWANA YESU
akushindie.
-Zishinde dhambi kwa kuondoka katika baraza
za watenda dhambi.
-Zishinde dhambi kwa kukaa mbali na picha za
ngono pamoja na kuangalia filamu za nusu uchi.
1 Yohana 2:15-17 '' Msiipende dunia, wala
mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda
dunia, kumpenda BABA hakumo ndani yake.
Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya
mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima,
havitokani na BABA, bali vyatokana na dunia.
Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali
yeye afanyaye mapenzi ya MUNGU adumu hata
milele. ''
-Ndugu yangu, kama YESU amenibadilisha
mimi kutoka dhambi zote mbaya unazozifahamu
nina hakika anaweza kukubadirisha hata wewe
ili ufanyike mtoto wa MUNGU kupitia yeye.
changamka ndugu kwani wakati wa wokovu ni
sasa.
Yohana 3:16-21 '' Kwa maana jinsi hii MUNGU
aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe
pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali
awe na uzima wa milele. Maana MUNGU
hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu
ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika
yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini
amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu
hakuliamini jina la Mwana pekee wa MUNGU. Na
hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja
ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko
nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.
Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia
nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake
yasije yakakemewa. Bali yeye aitendaye kweli
huja kwenye nuru, ili matendo yake yaonekane
wazi ya kuwa yametendwa katika MUNGU. ''
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi
tutajifunza tena siku nyingine.na kama
hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea
ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika
jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza
kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani.
MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki
upotelee motoni anataka uende uzimani aliko
KRISTO BWANA. MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
+255714252292
mabula1986@gmail.com
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.

WOKOVU NI ZAWADI BORA YA WANADAMU KUTOKA KWA MUNGU.


BWANA YESU atukuzwe.
Karibu nikujuze mipango ya MUNGU juu wa
wanadamu.
Wokovu ni zawadi bora kutoka kwa MUNGU kwa
ajili yetu wanadamu.
''Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia
ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi
zenu, ni kipawa cha MUNGU; wala si kwa
matendo, mtu awaye yote asije akajisifu. -
Waefeso 2:8-9''
Ukiupata wokovu unaingia kwenye familia ya
MUNGU.
Wokovu ni kumpokea YESU KRISTO.
Walio na wokovu Biblia inasema neno hili juu
yao. " Naye Alituokoa Katika Nguvu Za Giza,
Akatuhamisha Na Kutuingiza Katika Ufalme Wa
Mwana Wa Pendo Lake. Ambaye Katika Yeye
(YESU) Tuna Ukombozi, Yaani, Msamaha Wa
Dhambi- Wakolosai 1:13-14.
-Ni Furaha Kuu Kuwa Ndani Ya YESU KRISTO.
-Sio wote wamempokea BWANA YESU ila
ni faida kuu kumpokea BWANA YESU maana,
- Kumpokea YESU Ni Kuvuka Kutoka Mautini Na
Kuingia Uzimani.
'' Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele;
asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali
ghadhabu ya MUNGU inamkalia.Yohana 3:36''
YESU Akikuokoa ndugu yangu, Hata Ukiondoka
Duniani kama una Wokovu Wa BWANA YESU
Utakua Unaishi Paradiso(pema Peponi) Hata
Kama Walio Duniani Watakuwa Wanakuita
Marehemu.
-YESU KRISTO Ni Muhimu Kuliko Vyote
Unanavyovifahamu.
''Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu
na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na
kutusafisha na udhalimu wote. -1 Yohana 1:9''
Baada Ya Kifo Ni Hukumu. Neno Hilo Watu
Wengi Hawapendi Kulisikia Ila Ukweli Utabaki
Kuwa Ukweli lakini YESU KRISTO Anaokoa, Na
Kama Ukimpokea Unaokoka, Warumi 8:1-2
inasema '' Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu
juu yao walio katika KRISTO YESU. Kwa sababu
sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika KRISTO
YESU imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi
na mauti. ''
Ukiwa umempokea YESU KRISTO kama BWANA
na MWOKOZI wako MUNGU anakuambia
usiogope.
Hii ni ahadi kwa wateule wa MUNGU, Kwamba
tusiogope.
''Usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe,
usifadhaike, kwa maana mimi ni MUNGU wako
nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia naam,
mkono wa kuume wa haki yangu.Tazama wote
walioona hasira juu yako watatahayarika na
kufadhaika, watu washindanao nawe watakuwa
si kitu, na kuangamia. {Isaya 41:10-11}
Ndugu yangu, JEHOVAH MUNGU ana ushindi
wako, ana ushindi wako wa kuyashinda ya dunia
na ana ushindi wako wa kuwashinda kila
mawakala wa shetani ambao wanataka kukutoa
kwenye Wokovu wako. omba tu naye atajibu
maana yeye huliangalia neno lake ili alitimiz.
''Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda
ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili
kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na
uzima wa milele. -Yohana 3:16''
MUNGU akubariki sana kwa kujifunza ujumbe wa
leo. Na lengo la MUNGU ni kukuokoa mara tu
baada ya wewe kuijua kweli yake.
Kama unataka kuokoka omba kwa sauti yako
maombi haya kisha baada ya hapo jiunge na
kanisa la kiroho wanaoifundisha kweli ya
KRISTO. OMBA HIVI.
Eee BABA Wa Mbinguni, Ninakuja Kwako Katika
Jina La YESU KRISTO. Neno Lako Linasema "
Yeyote Ajaye Kwangu Sitamtupa Nje Kamwe-
Yohana 6:37." Basi Ninajua Kwamba BWANA
Hutanitupa Nje, Bali Utanipokea. Ninashukuru
Kwa Hili. Ulisema Katika Neno Lako Kwamba "
Ukimkiri YESU Kwa Kinywa Chako Ya Kuwa Ni
BWANA, Na Kuamini Moyoni Mwako Ya Kuwa
MUNGU Alimfufua Katika Wafu, UTAOKOKA,
Kwa Kuwa Kila Atakayeliitia Jina La BWANA
ATAOKOKA-Warumi 10:9,13". Ninaamini Kwa
Moyo Wangu Ya Kuwa YESU KRISTO Ni Mwana
Wa MUNGU. Nisamehe BWANA Dhambi Zangu
Zote, futa jina langu kwenye kitabu cha hukumu
na Liandike Jina Langu Kwenye Kitabu Chako
Cha Uzima. Ninaliitia Jina La YESU Na Ninajua
BABA Wa Mbinguni Unaniokoa Sasa. Neno Lako
Linasema " Kwa Moyo Mtu Huamini Hata Kupata
Haki, Na Kwa Kinywa Hukiri Hata Kupata
Wokovu-Warumi 10:10" Nimeamini Kwa Moyo
Wangu Na Ninamkiri BWANA YESU Sasa Na Kwa
Sababu Hii Nimeokolewa. Nafunga Ukurasa Wa
Dhambi Na Nafungua Ukurasa Wa Mema Tu
ROHO MTAKATIFU Nisaidie. Asante BWANA
YESU Kwa Kuniokoa. Kwa Jina La YESU KRISTO
Nimeomba. AMEN.
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi
tutajifunza tena siku nyingine.Endelea kuukulia
wokovu kwa mafundisho kanisani.
ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee
motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO
BWANA.
MUNGU akubariki sana
Ni mimi ndugu yako katika BWANA YESU.
Peter M Mabula
0714252292
Bali wote waliompokea(YESU KRISTO) aliwapa
uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio
wale waliaminio jina lake; -Yohana 1:12