Bwana Yesu asifiwe wana wa Mungu.....
Ev. Elimeleck Ndashikiwe
Nawapenda sana sana.
Fundisho hili linawahusu watu wote hususani wale wanaohudumu kanisani kwenye nafasi mbali mbali,
mfano waimbaji,
wakuu na viongozi wa idara mbali mbali,
pamoja na wale waliopo katika zile huduma tano
Waefeso 4:11.
Mpango wa Mungu sio kutoa adhabu kwa watu wake,
bali mpango wake ni kuwafanya watu kumtumikia Yeye tu kwa moyo,roho akili na nguvu zote.
Lakini panapo stahili kupata adhabu basi Mungu hasiti kuachilia adhabu sawa sawa na dhambi au kosa lillilopo.
Tukumbuke ya kwamba Mungu wetu sio dhalimu,
bali ni mwaminifu na mpole si mwepesi wa hasira naye ni mwingi wa huruma
Yoeli 2:13.
Hata hivyo tunakubaliana kwamba adhabu haiji bila kosa. Ikiwa mtu amekosa anapewa nafasi ya toba/kugeuka na kusamehewa mara moja.
Lakini anapoendelea kukosea kwa nia ya kupenda kukosea basi anastahili anyooshwe kwa adhabu,
ukizingatia kazi ya Mungu sio kazi ya kuchezea chezea wala sio kazi ya kuleta masihara.
Ikiwa umeitwa tu “mkristo” na umeokoka basi ujihesabu wewe ni mtumishi wa Mungu mahali ulipo,na uwe makini sana na njia
zako~
chunga unaongea nini!,
chunga marafiki zako ni akina nani ! Chunga unafanya nini!! N.K
“Adhabu ya kuliwa na chango madhabahuni”
Huu ni msamiati mgumu kwa sababu hata neno “chango” ni msamiati bado.
Hivyo neno “chango” ni aina fulani ya minyoo au wadudu wanaotafuna tumbo.
Sasa
kivipi minyoo ikawa ni adhabu kwa mkristo/mtumishi?
~ Kumbuka;
Bwana Mungu ana namna yake ya kuwanyoosha watu wake kwa adhabu pale inapostahili,
Yeye Mungu anaweza kufanya chochote kile kwa mtu yoyote yule.
Adhabu ya namna hii inakuja kwa mtu yule anayetwaa utukufu wa Mungu na kujilingalinisha
na Mungu mfano mzuri ni Herode yule aliyemuua Yakobo ndugu wa Yohana kwa upanga
(Matendo 12:1-4)
Biblia inatuambia;
“ Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi,
akatoa hotuba mbele yao.
Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu,
si sauti ya mwanadamu.
Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho.”
Matendo 12:21-23
Simulizi hii ya kifo cha Herode ni onyo kwa watu wote
wanaotwaa utukufu wa Mungu.
Herode hali akijua hotuba anayoitoa sio ya Mungu ni ya kwake lakini hakutaka kuonesha
hivyo bali alipendezwa na sauti za watu kuona yeye ni Mungu atoae hotuba.
Watu waliokuwa wakimsikiliza hawakuwa na ufahamu sahihi wa kuitambua sauti ya Mungu
bali yeye hali akijua sio sauti ya Mungu na hakutaka kumpa utukufu Mungu,Mungu akampiga kwa chango nao wakamla.
Hivyo Herode hakuuwawa na wanadamu bali Mungu mwenyewe kwa sababu hakutaka kumpa Mungu utukufu. Ikiwa kama hakutaka kumpa Mungu utukufu,basi ni
dhahiri mtu huyu alijiinua na kujifanya yeye ndio mungu mtu.
Kitu ambacho ni machukizo makubwa sana kwa Bwana ni kutwaa utukufu wake na kumpa mwingine,
kwa maana Bwana mwenyewe asema ;
“Mimi ni BWANA; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.”
Isaya 42:8
Leo hii nini kinaendelea madhabahuni?
Watu wengi wanapenda sifa na kujiinua ili watazamwe kuwa wao ni miungu watu.
Tena baadhi ya watu wanadiriki hata kusema
“Mungu kaniambia…”
na kumbe ndani yao wanashuhudiwa hawajaambiwa chochote kile,bali ni maneno yao wao wenyewe.
Hata kama ni kweli Bwana amekuambia,
swali la kujiuliza Je umeambiwa useme kwa wakati huo?
Haya na mengineyo mengi yanaendelea leo kwenye madhabahu ya Bwana. Hakika mimi
ninakuambia watu wa namna hii wanaojiiunua na kuchukua utukufu wa Mungu watapigwa na chango mpaka kufa kama
ilivyokuwa kwa Herode.!
Kuna adhabu ya kupigwa na chango kwa wale watakao iacha kweli wakajitwalia utukufu ambao utukufu huo ulitakiwa
uwe ni kwa Bwana tu.
Mimi nachelea kusema kila wakati neno hili “Bwana kaniambia…au Bwana kanisemesha...”
ikiwa sijaongea na Bwana kwa nini niseme uongo kwa nia ya kujiinua?
Sitaki kupigwa na adhabu ya chango!!!
~ Herode alikufa kimwili kwa kuliwa na minyoo ya gafula kama adhabu bali leo unaweza ukaliwa na magonjwa au ukaliwa kiroho
kiasi kwamba mbele za Mungu hakika ni umekufa hali kimwili upo hai. Ni hali mbaya sana hii!!!
Sio kila adhabu au majanga yote yanaletwa na shetani bali mengine ni adhabu ya Kiungu yenyewe
~ kuna wakati Mungu anaweza akaruhusu adhabu fulani mbaya kwenye maisha yako kwa sababu ya tabia ya kupenda kujiinua kwamba
unatwaa utukufu wa Mungu.
Wito wangu kwako wewe mkristo uliyeokoka ni kwamba,
epuka tabia ya kujitwalia utukufu wa Mungu.
Ikiwa Mungu amekutumia kwenye eneo lolote lile,
basi usiseme umefanya wewe kwa mikono yako bali sema Mungu ndie amefanya yote hayo,
na papo hapo kumbuka kuzikataa sauti za watu wanaokusifia bali kaza kusema ni Bwana tu ndie kayafanya yote.
Usijiinue kwa namna yoyote ile kwa maana usije ukafanana na Herode aliyepigwa na chango.
Ikiwa unaona unasumbuliwa na roho ya kujisifu fulani hivi,
au ikiwa una mtu anayekuumiza kwa tabia yake ya namna hii,
nawe hupendi awe nayo,
kwa maana hiyo roho ni ya rusifa/shetani basi
naomba usisite kunipigia simu kwa namba zangu hizi tuombe pamoja
+255715445846
+255684485460
Saturday, 10 June 2017
SOMO LA UONGOZI
Monday, 8 May 2017
WAKATI WA DHIKI KUU, KUIFIA IMANI
IMANI YA MTU NDIPO ITAKAPOINEKANA
Wakristo Wanaokufa kwa ajili ya Imani Mpinga Kristo atawatesa
wakati huu wa dhiki kuu.
Wakristo ambao watakuwa hawafuati mambo yake.
Hawatatii amri zake ila watendelea kuomba Mungu wa kweli wa taifa la Israeli
kupitia Masihi Yesu kristo.
Kwa ajili hii, wakristo watakuwa na uhusiano wa karibu na mwanamke Israeli
Ufu. 12:17.
Katika
Warumi 11:15-20.
Paulo anasema wakristo kutoka mataifa yasiyo ya kiyahudi wamefanywa kuwa sehemu ya mti wa mzeituni kwa hivyo,
wana uhusiano wa karibu sana nao.
Uhusiano huu ndio msingi wa mapenzi tuliyonayo
kwa watu wa taifa la Israeli.
Ombi letu ni kwamba wayahudi kutoka taifa la Israeli nao pia watamtambua Kristo kuwa mwokozi na kuingia katika mapatano naye
Heb. 8: 8-13.
Wakristo wa kweli watatambua mara moja
kwamba mpinga Kristo ni kiongozi wa uwongo.
Wao watamkataa,
pia watakataa kanisa lile la dunia atakaloanzisha.
Kwao, katika milki hii ya mnyama (the beast),
kuna njia moja tuu, nayo ni ile ya mateso na kufa kwa ajili ya Imani.
Kuhusu hawa watakaokufa kwa ajili ya imani yao,
Yohana anasema hivi:
"Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu,
na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.
Wakalia kwa sauti kuu,
wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutohukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?"
Ufu. 6:9-10.
Kati ya hawa watakaokufa kwa ajili ya imani,
watakuwa wale ambao wamekubali wokovu baada ya huduma kanisani kupitia kazi ya wayahudi 144,000, kutakuwa na wakristo kama hawa wengi.
Wao watajitoa kumpinga Kristo, na kuichua uongo wake.
Ikiwa wakati huu utakupata, jua kwamba wokovu wako hautahusika na kumpinga muovu,
na kukataa chapa yake, lakii haya yote yatategemea sana kumkubali Kristo.
Lazima utubu dhambi zako, mkubali Kristo awe Bwana wa maisha yako, na usafishwe na damu yake.
Ni kupitia haya utakuwa umejiandaa vyema
kumpinga huyu muovu, hata kama msimamo wako huu wa upinzani waweza kukufanya upoteze maisha yako.
Lazima uwe tayari kufa kwa ajili ya imani yako. Sababu ni kwamba waKristo hawatapona dhiki kuu:
"Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe,
wakaambiwa wastarehe bado mda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao"
(Ufu. 6:11).
Watakapofika mbinguni, hawa waliokufa kwa ajili ya imani yao watapewa mwili wa kufufuka,
nao watakuwa na furaha kuu pamoja na Mungu.
Hawatakumbuka shida na machozi ya mateso, njaa, na vifo kwa ajili ya imani. Kuhusu watakaofufuka,
Yohana anasema:
"Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu,
watu wa kila taifa, na kabila na jamaa, na
lugha wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele ya mwana kondoo wamevikwa mavazi meupe, wana matawi ya mitende
mikononi mwao…
Nikamwambia, Bwana wangu, wajua wewe.
Akaniambia, hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu, nao wamefua mavazi yao,
na kuyafanya meupe katika damu ya mwanakondoo…
Kwa maana huyo Mwana kondoo,
aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga,
naye atawaongoza kwenye chemi chemi za maji yenye uhai,
na Mungu atayafuta machozi yote katika macho yao"
Ufu. 7: 9, 14, 17.
Mkutano katika Mlima wa Mizeituni Kristo ataonekana mara ya pili hapa duniani
jinsi vile imeelezwa katika Ufu 19, na hii itakuwa pale katika mlima wa mizeituni.
Twasoma:
"Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa mizeituni,
unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki,
nao mlima wa mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi;
litakuwako huko bonde kubwa sana; nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini,
na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini.
Nanyi mtakimbia kwa njia ya bonde la milima yangu;
kwa maana bonde lile la milima litaenea hata Aseli;
naam, mtakimbia, kama vile mlivyokimbia mbele ya tetemeko la nchi, siku za Uzia,
mfalme wa Yuda; na Bwana, Mungu wangu, atakuja, na watakatifu wote pamoja naye"
Zek. 14:4-5.
Mwokozi wetu Kristo atakuja tena pamoja na watakatifu ambao walikuwa wameungana naye kwa muda wa miaka saba iliotangulia.
Sasa anakuja kuleta makubaliano (reconciled) na wale waliobaki taifa la Israeli
ambao wakati wa vita vya Har-Magedoni,
walikimbilia usalama katika sehemu zilizo na mawe kwenye mlima wa mizeituni.
Mkutano huu utakuwa kwa ajili ya kuwapa wokovu.
"Katika siku hiyo watu wa nyumba ya Daudi,
na wenyeji wa Yerusalemu, watafunguliwa chemchemi kwa dhambi na kwa unajisi"
(Zek. 13:1).
Pale wayahudi ambao wamepona wanapotaja alama za misumari mkononi na kuuliza:
"Na mtu atamwambia, J
e! jeraha hizi uizo nazo kati ya mkono yako ni nini?
naye atajibu,
Ni jeraha nilizotiwa katika nyumba ya rafiki zangu"
Zek. 13:6.
Huu utakuwa wakati mgumu kwani wayahudi
watajuta kwa ajli ya kutenda dhambi, na pia kwa ajili mababu zao walimkataa masihi wakati yeye alipokuja mara ya kwanza.
Katika Zekaria:
"Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi,
na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba;
nao watamtazama yeye ambaye walimchoma;
nao watamuombolezea, kama vile mtu amuombolezeaye mwanawe wa pekee;
nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.
Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu,
kama maombolezo ya Haddarimoni katika bonde la Megido"
(Zek. 12:10-11).
Kristo ataunganishwa na wale aliosafishwa,
wanaokimbia na wenye huzuni, naye atawatia moyo na maneno haya:
"Nami nitaleta fungu lile la tatu na kulipitisha
kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwayo,
nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo;
wataliita jina langu,nami nitawasikia; mimi nitasema,
watu hawa ndio wangu; nao watasema, Bwana
ndiye Mungu wangu"
(Zek. 13:9).
MUNGU WANGU WA MBINGUNI AKUBARIKI MSOMAJI WANGU,
Nakupenda sana ndo maana najitahidi kukushirikisha hiki kidogo.
Lakini pia, nikuombe, nitie moyo na unishike kwa mkono wako, ukiwa na chochote
kama sadaka kwa Bwana, ukiguswa nibariki pia.
Ndimi ndugu yako
Ev. Elimeleck S Ndashikiwe
Tel: +255767445846
+255715445846
WAKATI WA DHIKI KUU Sehemu ya III
HAPA NDIPO YULE ASI ATAKAPOJITOKEZA
Pale waIsraeli wanapobadili nia na kuanza kuwa tayari
kupokea wokovu, muovu hatachelewa kuchukua nafasi hii ili kujitoa wazi na kazi yake akiwa masihi wa uongo.
Baada ya kunyakuliwa wale walio na imani,
hofu kuu na wasi wasi itakumba taifa lote la Israeli.
Hali hii itazidishwa na vita pale Israeli itakaposhambuliwa na jeshi ambalo ni muungano
wa mataifa adui wa jadi.
Katika
Ezekieli 38 na 39.
Kwa njia ya miujiza kabisa, Mungu atajitokeza na kuwaokoa waIsraeli kwa njia ya ajabu.
Yeye atawaangamiza maadui wao. Na hapo hapo pia muyahudi mmoja atajitokeza na kuanza kufanya maajabu.
Yeye atapokea shukrani na sifa kimakosa kwani wengi wataamini kwamba yale Mungu amefanya kuokoa taifa la Israeli,
yamefanyika kwa ajili ya uwezo wake.
Atajitokeza na kusema kwamba ni yeye mwokozi wa Wayahudi,
na kwamba ni yeye amewaokoa waIsraeli,
na kwamba ni kutokana na uwezo wake taifa hili limeepuka bala kuu.
Yeye atasema kwamba ndiye Masihi baada ya majadiliano na mikutano viongozi wa taifa watamkubali kuwa ni yeye Masihi.
Mwokozi wetu Yesu Kristo anasema hivi kuhusu jambo hili:
"Nimekuja kwa jina la Baba, na hamjanipokea,
naye yule anayekuja kwa jina lake mwenyewe, enyi mumemupokea"
(Yoh. 5:43).
Huyu muongo ambaye atajaribu kumuiga Masihi na kujaribu kuchukua mahali pake,
ndiye yule ambaye anakuja akiwa amepanda farasi mweupe na ni yeye mpinga Kristo.
Naye hatakawia kujitengenezea makao yake akiwa kiongozi, na atawapa ruhusa waIsraeli
wajengee upya hekalu.
Yeye atafanyia mzaha wokovu ule wale Wayahudi 144,000 wamepokea na kusema kwamba msingi
wa
imani ya hawa 144,000 ni msingi wa uovu ulio kinyume cha mapenzi ya Mungu.
Na akiwa kinyume na mapenzi ya Bwana kuhusu ufufuo wa kiroho, yeye ataelekeza
yote yaliyo ya kiroho kwenye njia ya zamani
(orthodox)
ambayo itahusu kujenga upya hekalu na mwanzo mpya wa matumizi ya sherehe na kafara mbaya.
Kwa ajili ya sababu zilizo wazi hapa, wale
wayahudi ambao wamepokea wokovu wa kweli watakosa kusikilizana na hawa ambao
msingi wao ni huyu masiya wa uongo ambaye amejitokeza.
Hawa wafuasi wa masihi muongo ndio watakuwa wengi.
Hata pale atakapojitokeza na kwenda katika mataifa mbali mbali akijifanya kuwa masiya,
na hapo kuanzisha muungano wa kidini, wengi bado kwa ajili ya kutojua wataungana
naye na kumfuata, na kushiriki naye katika uovu wake.
KUTAKUWA NA MASHAHIDI WAWILI
Wakati huu ambapo kutakuwa na harakati kubwa sana za kuwapotosha waIsraeli,
Mungu atawatuma mashahidi wawili ili kueleza taifa la Israeli kwamba ni jambo la muhimu wao kurudi kwake Mungu wa kweli.
Ufunuo 11:3-12.
Kuna dalili katika maandishi matakatifu kwamba huenda hawa wawili wakawa
Musa na Eliya
ambao walionekaa na Kristo katika mlima tunaona
katika Mathayo 17:1-3.
Na kuhusu Eliya, katika mistari miwili ya mwisho wa Agano la Kale twasoma hivi:
"Angalieni, nitawapekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na kuogofya.
Naye ataigeuza mioyo ya Baba iwaelekee watoto wao,
na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana"
Mal. 4: 5-6.
Malkia wa Amani Abadilika na Kuwa Fidhuli Pale muda wa dhiki kuu utakapofikia kati kati, makubaliano kati ya waIsraeli na Masihi huyu wa uongo yatavunjika
pale yeye atakapojitangaza kwamba ni yeye Mungu katika hekalu.
2 The. 2:4
"Yule pingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa;
hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu."
Akisaidiwa na yule nabii wa uongo,
yeye atajenga na kutengeneza picha yake katika sehemu takatifu zaidi ya yote
katika hekalu, na kulazimisha kila mtu kumuabudu.
Yeye atatupilia mbali kila aina ya maombi
katika hekalu hata ule mtindo maalum wa kuomba ambao zawadi hutolewa kwa Mungu.
Danieli anasema hivi :
"Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja; na kwa nusu ya juma hiyo atakomesha sadaka na dhabihu;
na mahali pake litasimama chukizo la uharibifu;
na hivyo hata ukoma, na ghadhabu iliyokusudiwa imemwagwa juu yake mwenye kuharibu"
Dan. 9:27.
Kwa hivyo,
Danieli anasema wazi kwamba huyu mpinga Kristo atatupilia mbali utaratibu wa maombi ulioko na hata ule ambapo dhabihu
hutumiwa katika hekalu baada ya miaka tatu na nusu ya utawala wake.
Taifa lililo huzunika la Israeli litakataa kuendelea kumfuata huyu masihi wa uongo.
Taifa la Israeli ambalo limekasirishwa na huyu masihi wa uongo litakataa kumtii
huyu ambaye sasa atakuwa amejitangaza kuwa Mungu.
Na kwa ajili ya kufanya hivyo,
wao watamkasirisha huyu masihi wa uongo, naye atataka kukumbana nao na kuwaadhibu.
Yeye akiwa kama mungu atakuwa sawa na yule anayebebwa na yule farasi mwekundu.
Yeye atajitoa kupigana vita na kuangamiza taifa la Israeli na wote wale ambao si watiifu kwake na hawafuati mienendo yake.
Yeye atawaua mashahidi wawili ambao wamejitokeza na kuonya watu kuhusu uovu wake ( Ufunuo 11:7).
Pia yeye ataamuru wote walio na imani katika Kristo wauawe.
Kwa njia ya wazi kabisa, Kristo aliwaonya wayahudi kuhusu taabu itakayoletwa na huyu mpinga Kristo.
"Basi hapo mtakapoliona chukizo la uharibifu,
lile lililonenwa na nabii Danieli, imesimama katikl patakatifu (asomaye na afahamu) ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani; naye aliye juu ya
dari asishuke kuvichukua vitu vilivyomo nyumbani mwake;
wala aliye shambani asirudi nyuma kuichukua nguo yake.
Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo!
Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi,
wala siku ya sabato.
Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa ambayo haijatokea namna yake tangu
mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.
Na kama siku hizo zisingalifupizwa asingeokoka mtu yeyote; lakini kwa ajili ya wateule
zitafupizwa siku hizo"
Math 24:15-22.
Wakati huu wa dhiki kuu, Wayahudi wengi sana watauawa. Kuhusu jambo hili,
Zekaria anasema: "Hata, itakuwa ya kwamba katika nchi yote mafungu mawili yatakataliwa mbali.
Nao watakufa,
asema Bwana; lakini fungu la tatu litabaki humo"
Zek. 13:8.
Robo tatu itakayobaki itasafishwa na shida zile za dhiki, na pale Kristo atakaporudi,
kutakuwa na makubaliano naye.
Zekaria 13:9:
"Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha katika moto,
nami nitawasafisha kama fedha isafishwayo,
nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo;
wataliitia jina langu, nami nitawaasikia; mimi nitasema,
watu hawa ndio wangu;
nao watasema, BWANA ndiye Mungu wangu."
WATAKIMBIA HUKU NA HUKO
Ufunuo 12
WaIsraeli watakimbilia jangwani. Hii itatokea pale baada ya hekalu kuchafuliwa,
na kutupiliwa mbali kwa makubaliano kati ya taifa la Israeli na Masihi huyu muongo.
Hili ni tukio ambalo litatokea pale katikati ya muda ule wa dhiki kuu.
Katika Ufunuo 12
ugomvi mkuu kati ya waIsraeli na yule mpinga Kristo unazungumziwa kwa njia maalum,
na hii itakuwa kati ya Ufalme wa Mungu na ule wa shetani.
Yohana anasema hivi kuhusu vita:
"Na ishara kuu ilionekana mbinguni, mwanamke aliyevikwa jua,
na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na
juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili.
Naye alikuwa na mimba, akilia, hali ana uchungu na kuumwa katika kuzaa.
Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama,
joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake,
vilemba saba.
Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi.
Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili, azaapo,
amle mtoto wake.
Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakyewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma.
Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu,
na kwa kiti chake cha enzi.
Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotengenezwa na mungu,
ili wamlishe huko muda wa siku elfu na mia mbili sitini"
Ufu. 12:1-6.
Hapa taifa la Israeli lachukuliwa kuwa sawa na mama aliyeolewa,
sio kama mchumba bikira kama vile kanisa la Kristo lilivyo
(Yer. 31:1-5; Isa. 54:4-8; Hos. 2:15; Mat. 25:1-13; na 2 Kor. 11:2).
Huyu mwanamke anatajwa pia na kusemekana kuwa atakuwa na
nyota kumi na mbili
katika kichwa chake,
na hii ni alama ya makabila kumi na mbili ya Israeli,
pamoja na jua na mwezi ambavyo vimemlenga
Yakobo na Raheli
kama ni wao watu wa kwanza katika taifa la Israeli.
Haya yote yanaweza kulinganishwa na yale yaliyo
katika ndoto ya Yusufu katika Mwanzo ambapo tunasoma hivi:
"Akaota tena ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake,
akasema,
angalieni, nimeota ndoto nyingine;
na tazama, jua na mwezi na nyota kumi na moja zikaniinamia.
Akawambia baba yake na ndugu zake;
baba yake akamkemea akamwambia,
Ni ndoto gani hii uliyoiota?
Je! mimi na mama yako na ndugu zako tutakuja tukusujudie hata nchi?"
Mwa 37:9-10;
soma pia Yer. 31:11 na 15 ambapo Yakobo na Raheli wanachukuliwa kuwa kama taifa la Israeli).
Mimba ile ya mama huyu yaweza kuchukuliwa kumaanisha wakati ule wa kuzaliwa Kristo.
Yule mnyama ambaye anajiweka tayari kumla mtoto anapozaliwa bila shaka ni muovu shetani mwenyewe.
Wakati huu, mfalme muovu ni yule Herode.
Ndiye aliyeamua kwamba watoto wote wakiume
wauliwe ili mwokozi wetu Yesu Kristo auliwe.
Hata hivyo Mungu alikuja na kutenda kazi
ya ajabu hapa duniani pale alipofanya kazi yake kuu na kurudi mbinguni kwake BABA yetu aliye Juu.
Muda wake ule wa kutawala na nguvu kabisa utaanza pale atakaporudi mara ya pili.
Ufunuo 2:26-27.
Mpaka pale Kristo atakapokuja tena, muovu shetani anaelekeza nguvu zake zote
kujaribu kupinga ufalme wa Mungu, taifa la Israeli na kanisa.
Baada ya kanisa kunyakuliwa,
yeye sasa atalipatia nguvu zake kwa taifa la Israeli,
kwanza kuhadaa, na baadaye kuangamiza taifa la Israeli ili mpango wa Mungu utimizwe.
Ni wakati huu taifa la Israeli litaamriwa kukimbilia jangwani,
labda kukimbilia Petra ili kuepuka dhiki kuu.
Huko Mungu atawalinda kwa muda wa siku 1260,
ambazo ni kama miaka tatu na nusu.
Hii tunaiita ile miaka mitatu na nusu ya kwanza ya utawala wa mpibgs Kristo,
Itakuwa miaka yautawala wa amani.
Barikiwa sana mpendwa wangu
Guatana nsmi tu usichoke......
Ni mimi ndugu yako
Ev. Elimeleck S Ndashikiwe