Pages

Subscribe:

Friday, 6 September 2019

KANUNI ZA KIROHO By Ev. Elimeleck Ndashikiwe

    Kila jambo maishani lina kanuni zake.
Kadhalika maisha ya kiroho yana kanuni zake za jinsi ya kushirikiana na Mungu.

     1. MWENYEZI MUNGU ANAKUPENDA, NAYE ANATAKA KUKUPANGIA MPANGO WA AJABU KWA MAISHA YAKO.

       UPENDO WA MUNGU
  Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
       Yohana 3:16

MPANGO WA MUNGU KWAKO
      Mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.
Yohana 10:10

      Je, kwa nini watu wengi hawana uzima huo? Ni kwa sababu . . .

      2. MWANADAMU NI MWENYE DHAMBI.
       Dhambi zake zimemtenga na Mungu.Kwa hiyo hajui upendo na mpango wa Mungu kwa maisha yake.

      MWANADAMU NI MWENYE DHAMBI
Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
        Warumi 3:23

    Mungu alimwumba mwanadamu kwa kusudi la kushirikiana naye, lakini mwanadamu alikwenda kinyume cha mpango wa Mungu.
     Alichagua kumwasi Mungu badala ya kumtii.
  Kumwasi Mungu ni kufanya dhambi.

       Mtu anapoishi kinyume cha mapenzi ya Mungu anaendelea kuishi maisha ya dhambi.

      MWANADAMU AMETENGANA NA MUNGU
    Lakini maovu yenu yamewatenga ninyi na Mungu wenu.
        Isaya 59:2

       Mungu Mtakatifu hana ushirika na dhambi.
       Kati yake na mwanadamu kuna ufa mkubwa wa dhambi.
    Mwanadamu hujaribu kumfikia Mungu kwa nija nyingi:
   dini, matendo mema, sala, n.k., lakini hizi zote hazitoshi.

     Mwanadamu bado ni mwenye dhambi. Kuna njia moja tu ya kushirikiana na Mungu . .

      3. YESU KRISTO NI NJIA YA PEKEE YA KUONDOA DHAMBI.
     Alikufa kwa ajili yetu ili tujue upendo na mpango wa Mungu kwa maisha yetu.
        ALIKUFA ILI ATULETE KWA MUNGU
Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu.
        1 Petro 3:18

      YESU YU HAI
Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yanenavyo maandiko; na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alitufuka siku ya tatu,
     kama yanenavyojil maandiko.
      1 Wakorintho 15:3,4

YESU NDIYE NJIA YA PEKEE
       Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
           Yohana 14:6

      Mwanadamu peke yake hawezi kushirikiana na Mungu. Mungu alimtuma Yesu afe msalabani kwa ajili ya dhambi zetu na tena awe daraja kati yetu na Mungu ili atulete kwa Mungu.

      Sasa kanuni ya nne itakuambia jinsi uwezavyo kumjua maishani mwako . . .

    4. INAKUPASA KUMPOKEA YESU AWE MWOKOZI NA MTAWALA WAKO.
         Ndipo utajua upendo na mpango wa Mungu kwa maisha yako.

   UNAMPOKEA KRISTO KWA IMANI
Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.
        Yohana 1:12

   Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.
Waefeso 2:8,9

     INAKUPASA KUMKARIBISHA YESU, MAISHANI MWAKO
     Ndashikiwe
nasimama milangoni, nabisha, mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake . . .

    Kumpokea Yesu Kristo ni:
Kujua wewe ni mwenye dhambi na kugeuka nafsi yako kwa Mungu na kutubu.
      Kumtegemea Mungu kwa kukusamehe kabisa.

   MUNGU WANGU WA MBINGUNI AWABARIKI SANA TENA SANA

   By Ev. Elimeleck Ndashikiwe

    Tel: +255762 680 380

USHINDI

HUWEZI KUWA SHUJAA IKIWA AU USIPOSHINDANA NA UKASHINDA

          Mungu wetu ni mwaminifu wakati wote, anatupatia nguvu ya kushinda na kuweza.

ISAYA 7:14 Yeye ni shujaa anayo mamlaka, uweza na nguvu kutufanikisha ktk hatua zetu zote

MWAMINI YEYE NAWE UTADHIBITIKA, WAHESHIMU NA WATUMISHI WAKE UTAINULIWA.

Thursday, 18 October 2018

UNGEPENDA KUFAHAMU MIMI NI NANI? Kwa ufupi tu

Hii nayo ni sehemu ya USHUHUDA wangu mbele za mataifa yote kwa zawadi hii aliyonipatia MUNGU.
Nikiwa ktk moja ya huduma za Kiroho ikiwa ni kipawa cha Mungu juu yangu
Huyu ndiye mama yetu Mzazi aliyetumiwa na Mungu kutufikisha hapa tulipo. Mungu amzidishie ktk kila alichonacho na afya njema.
Mungu ni mwema hakika, ametuweka karibu na pamoja na wtu wengine pia

Bwana Yesu Kristo asifiwe sana ndugu yangu Mpendwa, SIKU zote maisha ni hatua,

     Aliyeniona Jana anaweza kuniona wa tofauti akibahatika tena kuniona Leo au hata Kesho na Kesho Kutwa yake.

     Kadri siku zinavyozidi kubadilika Leo na Kesho, maisha nayo yanabadilika, umri nao unabadilika, afya nayo kimaumbile inabadilika pia,

     Lakini yote haya tunayatambua kuwa ni nyakati na majira ya Bwana aliyoyaweka kwa ajili yangu na hata kwa mtu mwingine yeyote.

KILA KIUMBE CHENYE UHAI KINAKUA, KINAONGEZEKA NA CHAWEZA KUPUNGUA PIA,

Lakini kinaposhindwa kukua wala kubadilika, basi hicho kitakuwa kimedumaa au kimekufa kabisa.

Binafsi namshukuru MUNGU wangu wa Mbinguni ananilinda na kunihuisha kila iitwapo Leo na kesho, nafurahia tu tena saaaaaana........

HISTORIA YANGU KWA UFUPI
         Majina yangu kamili naitwa ELIMELECK SIMON NDASHIKIWE

Ni mtoto wa pekee mzaliwa wa kwanza kati ya watoto sita (6) wa baba yetu
Mzee SIMON L NDASHIKIWE ambaye ktk ujana wake wote amemtumikia Mungu akiwa ni MCHUNGAJI WA KANISA LA KRISTO,

      Akiwa pamoja na mama yetu mzazi aitwaye ELINA KABABA SINDUHIJE,

Wazazi wetu wote hawa wamezaliwa Mkoani KIGOMA, wilaya ya KASULU katika kijiji cha KWAGA.

........nasi yangu tukiwa watoto wadogo tumekulia Kule na kupata Elimu ya msingi katika
SHULE YA MSINGI KWAGA,

   ,......na elimu ya Sekondari nimeipata katika SHULE YA SEKONDARI UJIJI - KIGOMA.

      Wazazi wetu hawa wametumika sehemu kadha wa kadha chini ya Dhehebu la
EVANGELISTIC ASSEMBLIES OF GOD (T) hadi Leo hii.

(Nisiwazungumzie sana wazazi...).

        Mimi kama mzaliwa wa kwanza ktk familia ya Pastor SIMON NDASHIKIWE, nimepata Neema ya kuwa lango nikiwa na wadogo zangu watano (5),
Wawili wa kike ambao ni
   . PRICILLA S NDASHIKIWE
   . ESTHER S NDASHIKIWE

Watatu wa kiume ambao ni
   . ISACK S NDASHIKIWE
   . PAULO S NDASHIKIWE na
   . AMOS S NDASHIKIWE

NB:
      Tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu wetu wa Mbinguni kutupatia kibali hiki cha kuzaliwa ktk familia ya MLAWI,

Nasi pia kama watoto, ni shauku yetu kumtumikia Mungu na kumpenda kwa mioyo yetu yote.

         Yako mengi ambayo ametutendea
na hata sasa bado anatenda.

         Asante sana Mungu kwa Bwana wetu Yesu Kristo kwa kutufanya kuwa WATOTO WA MUNGU.

         Ni MAOMBI yetu ya dhati kabisa
uzidi kuwalinda wazazi wetu na kuwapa afya NJEMA na uwatie nguvu katika kazi yako ya Utumishi  (UCHUNGAJI).

    SIFA, HESHIMA NA UTUKUFU
VIKURUDIE WEWE UWEZAYE KUTENDA MAMBO MAKUBWA NA YA AJABU ZAIDI YA YALE YOTE
TUYAWAZAYO NA KUYAOMBA.........!

EFES 3:20.........

                               AMEEEN.