Pages

Subscribe:

Monday, 8 May 2017

WAKATI WA DHIKI KUU, KUIFIA IMANI

IMANI YA MTU NDIPO ITAKAPOINEKANA

Wakristo Wanaokufa kwa ajili ya Imani Mpinga Kristo atawatesa
wakati huu wa dhiki kuu.

Wakristo ambao watakuwa hawafuati mambo yake.
Hawatatii amri zake ila watendelea kuomba Mungu wa kweli wa taifa la Israeli
kupitia Masihi Yesu kristo.

Kwa ajili hii, wakristo watakuwa na uhusiano wa karibu na mwanamke Israeli
Ufu. 12:17.

Katika
Warumi 11:15-20.
Paulo anasema wakristo kutoka mataifa yasiyo ya kiyahudi wamefanywa kuwa sehemu ya mti wa mzeituni kwa hivyo,
wana uhusiano wa karibu sana nao.

Uhusiano huu ndio msingi wa mapenzi tuliyonayo
kwa watu wa taifa la Israeli.

Ombi letu ni kwamba wayahudi kutoka taifa la Israeli nao pia watamtambua Kristo kuwa mwokozi na kuingia katika mapatano naye
Heb. 8: 8-13.

Wakristo wa kweli watatambua mara moja
kwamba mpinga Kristo ni kiongozi wa uwongo.

Wao watamkataa,
pia watakataa kanisa lile la dunia atakaloanzisha.
Kwao, katika milki hii ya mnyama (the beast),

kuna njia moja tuu, nayo ni ile ya mateso na kufa kwa ajili ya Imani.

Kuhusu hawa watakaokufa kwa ajili ya imani yao,
Yohana anasema hivi:

"Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu,
na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.
Wakalia kwa sauti kuu,
wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutohukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?"
Ufu. 6:9-10.

Kati ya hawa watakaokufa kwa ajili ya imani,
watakuwa wale ambao wamekubali wokovu baada ya huduma kanisani kupitia kazi ya wayahudi 144,000, kutakuwa na wakristo kama hawa wengi.

Wao watajitoa kumpinga Kristo, na kuichua uongo wake.
Ikiwa wakati huu utakupata, jua kwamba wokovu wako hautahusika na kumpinga muovu,
na kukataa chapa yake, lakii haya yote yatategemea sana kumkubali Kristo.

Lazima utubu dhambi zako, mkubali Kristo awe Bwana wa maisha yako, na usafishwe na damu yake.
Ni kupitia haya utakuwa umejiandaa vyema
kumpinga huyu muovu, hata kama msimamo wako huu wa upinzani waweza kukufanya upoteze maisha yako.

Lazima uwe tayari kufa kwa ajili ya imani yako. Sababu ni kwamba waKristo hawatapona dhiki kuu:

"Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe,
wakaambiwa wastarehe bado mda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao"
(Ufu. 6:11).

Watakapofika mbinguni, hawa waliokufa kwa ajili ya imani yao watapewa mwili wa kufufuka,
nao watakuwa na furaha kuu pamoja na Mungu.

Hawatakumbuka shida na machozi ya mateso, njaa, na vifo kwa ajili ya imani. Kuhusu watakaofufuka,

          Yohana anasema:
"Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu,
watu wa kila taifa, na kabila na jamaa, na
lugha wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele ya mwana kondoo wamevikwa mavazi meupe, wana matawi ya mitende
mikononi mwao…

Nikamwambia, Bwana wangu, wajua wewe.
Akaniambia, hao ndio wanatoka katika dhiki ile iliyo kuu, nao wamefua mavazi yao,
na kuyafanya meupe katika damu ya mwanakondoo…

Kwa maana huyo Mwana kondoo,
aliye katikati ya kiti cha enzi, atawachunga,

naye atawaongoza kwenye chemi chemi za maji yenye uhai,
na Mungu atayafuta machozi yote katika macho yao"
Ufu. 7: 9, 14, 17.

Mkutano katika Mlima wa Mizeituni Kristo ataonekana mara ya pili hapa duniani
jinsi vile imeelezwa katika Ufu 19, na hii itakuwa pale katika mlima wa mizeituni.

Twasoma:
"Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa mizeituni,
unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki,
nao mlima wa mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi;

litakuwako huko bonde kubwa sana; nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini,
na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini.

Nanyi mtakimbia kwa njia ya bonde la milima yangu;
kwa maana bonde lile la milima litaenea hata Aseli;

naam, mtakimbia, kama vile mlivyokimbia mbele ya tetemeko la nchi, siku za Uzia,
mfalme wa Yuda; na Bwana, Mungu wangu, atakuja, na watakatifu wote pamoja naye"
Zek. 14:4-5.

Mwokozi wetu Kristo atakuja tena pamoja na watakatifu ambao walikuwa wameungana naye kwa muda wa miaka saba iliotangulia.
Sasa anakuja kuleta makubaliano (reconciled) na wale waliobaki taifa la Israeli

ambao wakati wa vita vya Har-Magedoni,

walikimbilia usalama katika sehemu zilizo na mawe kwenye mlima wa mizeituni.
Mkutano huu utakuwa kwa ajili ya kuwapa wokovu.

"Katika siku hiyo watu wa nyumba ya Daudi,
na wenyeji wa Yerusalemu, watafunguliwa chemchemi kwa dhambi na kwa unajisi"
(Zek. 13:1).

Pale wayahudi ambao wamepona wanapotaja alama za misumari mkononi na kuuliza:
"Na mtu atamwambia, J
e! jeraha hizi uizo nazo kati ya mkono yako ni nini?
naye atajibu,
Ni jeraha nilizotiwa katika nyumba ya rafiki zangu"
Zek. 13:6.

Huu utakuwa wakati mgumu kwani wayahudi
watajuta kwa ajli ya kutenda dhambi, na pia kwa ajili mababu zao walimkataa masihi wakati yeye alipokuja mara ya kwanza.

Katika Zekaria:
"Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi,
na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba;

nao watamtazama yeye ambaye walimchoma;
nao watamuombolezea, kama vile mtu amuombolezeaye mwanawe wa pekee;

nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.

Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu,
kama maombolezo ya Haddarimoni katika bonde la Megido"
(Zek. 12:10-11).

Kristo ataunganishwa na wale aliosafishwa,
wanaokimbia na wenye huzuni, naye atawatia moyo na maneno haya:

"Nami nitaleta fungu lile la tatu na kulipitisha
kati ya moto, nami nitawasafisha kama fedha isafishwayo,
nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo;
wataliita jina langu,nami nitawasikia; mimi nitasema,
watu hawa ndio wangu; nao watasema, Bwana
ndiye Mungu wangu"
(Zek. 13:9).






MUNGU WANGU WA MBINGUNI AKUBARIKI MSOMAJI WANGU,

Nakupenda sana ndo maana najitahidi kukushirikisha hiki kidogo.

Lakini pia, nikuombe, nitie moyo na unishike kwa mkono wako, ukiwa na chochote
kama sadaka kwa Bwana, ukiguswa nibariki pia.

Ndimi ndugu yako
           Ev. Elimeleck S Ndashikiwe

Tel: +255767445846
        +255715445846

WAKATI WA DHIKI KUU Sehemu ya III

HAPA NDIPO YULE ASI ATAKAPOJITOKEZA

Pale waIsraeli wanapobadili nia na kuanza kuwa tayari
kupokea wokovu, muovu hatachelewa kuchukua nafasi hii ili kujitoa wazi na kazi yake akiwa masihi wa uongo.

Baada ya kunyakuliwa wale walio na imani,
hofu kuu na wasi wasi itakumba taifa lote la Israeli.

Hali hii itazidishwa na vita pale Israeli itakaposhambuliwa na jeshi ambalo ni muungano
wa mataifa adui wa jadi.

Katika
Ezekieli 38 na 39.
Kwa njia ya miujiza kabisa, Mungu atajitokeza na kuwaokoa waIsraeli kwa njia ya ajabu.

Yeye atawaangamiza maadui wao. Na hapo hapo pia muyahudi mmoja atajitokeza na kuanza kufanya maajabu.

Yeye atapokea shukrani na sifa kimakosa kwani wengi wataamini kwamba yale Mungu amefanya kuokoa taifa la Israeli,
yamefanyika kwa ajili ya uwezo wake.

Atajitokeza na kusema kwamba ni yeye mwokozi wa Wayahudi,
na kwamba ni yeye amewaokoa waIsraeli,
na kwamba ni kutokana na uwezo wake taifa hili limeepuka bala kuu.

Yeye atasema kwamba ndiye Masihi baada ya majadiliano na mikutano viongozi wa taifa watamkubali kuwa ni yeye Masihi.
Mwokozi wetu Yesu Kristo anasema hivi kuhusu jambo hili:

"Nimekuja kwa jina la Baba, na hamjanipokea,
naye yule anayekuja kwa jina lake mwenyewe, enyi mumemupokea"
(Yoh. 5:43).

Huyu muongo ambaye atajaribu kumuiga Masihi na kujaribu kuchukua mahali pake,
ndiye yule ambaye anakuja akiwa amepanda farasi mweupe na ni yeye mpinga Kristo.

Naye hatakawia kujitengenezea makao yake akiwa kiongozi, na atawapa ruhusa waIsraeli
wajengee upya hekalu.

Yeye atafanyia mzaha wokovu ule wale Wayahudi 144,000 wamepokea na kusema kwamba msingi
wa
imani ya hawa 144,000 ni msingi wa uovu ulio kinyume cha mapenzi ya Mungu.

Na akiwa kinyume na mapenzi ya Bwana kuhusu ufufuo wa kiroho, yeye ataelekeza
yote yaliyo ya kiroho kwenye njia ya zamani
(orthodox)

ambayo itahusu kujenga upya hekalu na mwanzo mpya wa matumizi ya sherehe na kafara mbaya.

Kwa ajili ya sababu zilizo wazi hapa, wale
wayahudi ambao wamepokea wokovu wa kweli watakosa kusikilizana na hawa ambao
msingi wao ni huyu masiya wa uongo ambaye amejitokeza.
Hawa wafuasi wa masihi muongo ndio watakuwa wengi.

Hata pale atakapojitokeza na kwenda katika mataifa mbali mbali akijifanya kuwa masiya,
na hapo kuanzisha muungano wa kidini, wengi bado kwa ajili ya kutojua wataungana
naye na kumfuata, na kushiriki naye katika uovu wake.

KUTAKUWA NA MASHAHIDI WAWILI

Wakati huu ambapo kutakuwa na harakati kubwa sana za kuwapotosha waIsraeli,
Mungu atawatuma mashahidi wawili ili kueleza taifa la Israeli kwamba ni jambo la muhimu wao kurudi kwake Mungu wa kweli.

        Ufunuo 11:3-12.
Kuna dalili katika maandishi matakatifu kwamba huenda hawa wawili wakawa
Musa na Eliya
ambao walionekaa na Kristo katika mlima tunaona
katika Mathayo 17:1-3.

Na kuhusu Eliya, katika mistari miwili ya mwisho wa Agano la Kale twasoma hivi:
"Angalieni, nitawapekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na kuogofya.
Naye ataigeuza mioyo ya Baba iwaelekee watoto wao,
na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana"
Mal. 4: 5-6.

Malkia wa Amani Abadilika na Kuwa Fidhuli Pale muda wa dhiki kuu utakapofikia kati kati, makubaliano kati ya waIsraeli na Masihi huyu wa uongo yatavunjika
pale yeye atakapojitangaza kwamba ni yeye Mungu katika hekalu.

         2 The. 2:4
"Yule pingamizi, ajiinuaye nafsi yake juu ya kila kiitwacho Mungu ama kuabudiwa;
hata yeye mwenyewe kuketi katika hekalu la Mungu, akijionyesha nafsi yake kana kwamba yeye ndiye Mungu."

Akisaidiwa na yule nabii wa uongo,
yeye atajenga na kutengeneza picha yake katika sehemu takatifu zaidi ya yote
katika hekalu, na kulazimisha kila mtu kumuabudu.

Yeye atatupilia mbali kila aina ya maombi
katika hekalu hata ule mtindo maalum wa kuomba ambao zawadi hutolewa kwa Mungu.

Danieli anasema hivi :

"Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja; na kwa nusu ya juma hiyo atakomesha sadaka na dhabihu;
na mahali pake litasimama chukizo la uharibifu;
na hivyo hata ukoma, na ghadhabu iliyokusudiwa imemwagwa juu yake mwenye kuharibu"
Dan. 9:27.

Kwa hivyo,
Danieli anasema wazi kwamba huyu mpinga Kristo atatupilia mbali utaratibu wa maombi ulioko na hata ule ambapo dhabihu
hutumiwa katika hekalu baada ya miaka tatu na nusu ya utawala wake.

Taifa lililo huzunika la Israeli litakataa kuendelea kumfuata huyu masihi wa uongo.

Taifa la Israeli ambalo limekasirishwa na huyu masihi wa uongo litakataa kumtii
huyu ambaye sasa atakuwa amejitangaza kuwa Mungu.

Na kwa ajili ya kufanya hivyo,
wao watamkasirisha huyu masihi wa uongo, naye atataka kukumbana nao na kuwaadhibu.

Yeye akiwa kama mungu atakuwa sawa na yule anayebebwa na yule farasi mwekundu.
Yeye atajitoa kupigana vita na kuangamiza taifa la Israeli na wote wale ambao si watiifu kwake na hawafuati mienendo yake.

Yeye atawaua mashahidi wawili ambao wamejitokeza na kuonya watu kuhusu uovu wake ( Ufunuo 11:7).

Pia yeye ataamuru wote walio na imani katika Kristo wauawe.
Kwa njia ya wazi kabisa, Kristo aliwaonya wayahudi kuhusu taabu itakayoletwa na huyu mpinga Kristo.

"Basi hapo mtakapoliona chukizo la uharibifu,
lile lililonenwa na nabii Danieli, imesimama katikl patakatifu (asomaye na afahamu) ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani; naye aliye juu ya
dari asishuke kuvichukua vitu vilivyomo nyumbani mwake;

wala aliye shambani asirudi nyuma kuichukua nguo yake.

Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo!
Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi,
wala siku ya sabato.

Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa ambayo haijatokea namna yake tangu
mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.

Na kama siku hizo zisingalifupizwa asingeokoka mtu yeyote; lakini kwa ajili ya wateule
zitafupizwa siku hizo"
Math 24:15-22.

Wakati huu wa dhiki kuu, Wayahudi wengi sana watauawa. Kuhusu jambo hili,
Zekaria anasema: "Hata, itakuwa ya kwamba katika nchi yote mafungu mawili yatakataliwa mbali.
Nao watakufa,
asema Bwana; lakini fungu la tatu litabaki humo"
Zek. 13:8.

Robo tatu itakayobaki itasafishwa na shida zile za dhiki, na pale Kristo atakaporudi,
kutakuwa na makubaliano naye.

         Zekaria 13:9:
"Nami nitalileta fungu lile la tatu na kulipitisha katika moto,
nami nitawasafisha kama fedha isafishwayo,
nami nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo;

wataliitia jina langu, nami nitawaasikia; mimi nitasema,
watu hawa ndio wangu;
nao watasema, BWANA ndiye Mungu wangu."

WATAKIMBIA HUKU NA HUKO

        Ufunuo 12
WaIsraeli watakimbilia jangwani. Hii itatokea pale baada ya hekalu kuchafuliwa,
na kutupiliwa mbali kwa makubaliano kati ya taifa la Israeli na Masihi huyu muongo.

Hili ni tukio ambalo litatokea pale katikati ya muda ule wa dhiki kuu.

Katika Ufunuo 12
ugomvi mkuu kati ya waIsraeli na yule mpinga Kristo unazungumziwa kwa njia maalum,
na hii itakuwa kati ya Ufalme wa Mungu na ule wa shetani.

Yohana anasema hivi kuhusu vita:

"Na ishara kuu ilionekana mbinguni, mwanamke aliyevikwa jua,
na mwezi ulikuwa chini ya miguu yake, na
juu ya kichwa chake taji ya nyota kumi na mbili.

Naye alikuwa na mimba, akilia, hali ana uchungu na kuumwa katika kuzaa.

Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama,
joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake,
vilemba saba.

Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi.

Na yule joka akasimama mbele ya yule mwanamke aliye tayari kuzaa, ili, azaapo,
amle mtoto wake.

Naye akazaa mtoto mwanamume, yeye atakyewachunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma.

Na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu,
na kwa kiti chake cha enzi.

Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali palipotengenezwa na mungu,
ili wamlishe huko muda wa siku elfu na mia mbili sitini"
Ufu. 12:1-6.

Hapa taifa la Israeli lachukuliwa kuwa sawa na mama aliyeolewa,
sio kama mchumba bikira kama vile kanisa la Kristo lilivyo
(Yer. 31:1-5; Isa. 54:4-8; Hos. 2:15; Mat. 25:1-13; na 2 Kor. 11:2).

Huyu mwanamke anatajwa pia na kusemekana kuwa atakuwa na
nyota kumi na mbili
katika kichwa chake,

na hii ni alama ya makabila kumi na mbili ya Israeli,

pamoja na jua na mwezi ambavyo vimemlenga
Yakobo na Raheli
kama ni wao watu wa kwanza katika taifa la Israeli.

Haya yote yanaweza kulinganishwa na yale yaliyo
katika ndoto ya Yusufu katika Mwanzo ambapo tunasoma hivi:

"Akaota tena ndoto nyingine, akawaambia ndugu zake,
akasema,

angalieni, nimeota ndoto nyingine;
na tazama, jua na mwezi na nyota kumi na moja zikaniinamia.

Akawambia baba yake na ndugu zake;
baba yake akamkemea akamwambia,

Ni ndoto gani hii uliyoiota?
Je! mimi na mama yako na ndugu zako tutakuja tukusujudie hata nchi?"

Mwa 37:9-10;

soma pia Yer. 31:11 na 15 ambapo Yakobo na Raheli wanachukuliwa kuwa kama taifa la Israeli).

Mimba ile ya mama huyu yaweza kuchukuliwa kumaanisha wakati ule wa kuzaliwa Kristo.

Yule mnyama ambaye anajiweka tayari kumla mtoto anapozaliwa bila shaka ni muovu shetani mwenyewe.

Wakati huu, mfalme muovu ni yule Herode.

Ndiye aliyeamua kwamba watoto wote wakiume
wauliwe ili mwokozi wetu Yesu Kristo auliwe.

Hata hivyo Mungu alikuja na kutenda kazi
ya ajabu hapa duniani pale alipofanya kazi yake kuu na kurudi mbinguni kwake BABA yetu aliye Juu.

Muda wake ule wa kutawala na nguvu kabisa utaanza pale atakaporudi mara ya pili.
Ufunuo 2:26-27.

Mpaka pale Kristo atakapokuja tena, muovu shetani anaelekeza nguvu zake zote
kujaribu kupinga ufalme wa Mungu, taifa la Israeli na kanisa.

Baada ya kanisa kunyakuliwa,
yeye sasa atalipatia nguvu zake kwa taifa la Israeli,
kwanza kuhadaa, na baadaye kuangamiza taifa la Israeli ili mpango wa Mungu utimizwe.

Ni wakati huu taifa la Israeli litaamriwa kukimbilia jangwani,
labda kukimbilia Petra ili kuepuka dhiki kuu.

Huko Mungu atawalinda kwa muda wa siku 1260,
ambazo ni kama miaka tatu na nusu.

Hii tunaiita ile miaka mitatu na nusu ya kwanza ya utawala wa mpibgs Kristo,

Itakuwa miaka yautawala wa amani.

Barikiwa sana mpendwa wangu

Guatana nsmi tu usichoke......

Ni mimi ndugu yako
           Ev. Elimeleck S Ndashikiwe

WAKATI WA DHIKI KUU DUNIANI Sehemu ya II

WIKI MOJA YA DHIKI KUU

Katika taifa la kiyahudi Israeli,
wana mtindo wa kuhesabu ambapo nambari saba inatumika sana.

Kwa mfano baada ya siku saba,
hii ni wiki moja,
baada ya miaka sita, mwaka wa saba ni mwaka maalum,
mwaka wa sabato, na baada ya miaka saba mara saba,

mwaka wa hamsini (jubilee) huwa ni mwaka maalum wa sherehe.

         Walawi 25:1-10
Na kwa vile dhiki kuu na kudumu kwa muda wa miaka saba,
jinsi vile tunasoma katika

Dan 9:27
kuna umuhimu wa kutilia maanani sana jinsi vile wayahudi huhesabu siku na miaka yao.

Mwaka wa mwisho kabla ya mwaka maalum wa hamsini unaotangulia kurudi kwa
Masihi utakuwa wakati wa majaribu mengi na msisimko wa kiroho katika taifa la wayahudi.

Taifa hili bado limefunikwa macho, na mengi yatalikumba wakati wa miaka ile saba ya dhiki

(soma Yer. 30:7; Dan. 9:27; Eze. 22:19-21; Zek.13:8-9).

Baada ya muda huu wa taabu na kujibadili,
taifa la Wayahudi litaingia kwenye utaratibu maalum wa taifa kuu la wateule ambao wataokoloewa kutoka kwa maafa ya dhiki kuu.

Kutakuwa na muamko wa kiroho katika taifa hili baada ya miaka hiyo saba.
Ni
kutokana na jinsi wayahudi wanahesabu miaka na siku ndipo tunapata uhakika kwamba kweli dhiki kuu itachukua miaka saba.

Hata Danieli anataja haya katika
Dan 9:27

Miaka ya mwisho ya dhiki hii itachukua miezi 42 ambayo ni sawa na siku 1260. Kwa hivyo,
tunaweza kusema haya: ·

Kutakuwa na watumishi wa Mungu maalum wawili ambao watafanya kazi ya Bwana kwa muda wa siku 1260 wakati wa dhiki kuu
(soma Ufu.11:3). ·

Hekalu kuu ya Yerusalemu itaharibiwa na kuchafuliwa kwa muda wa miezi 42 (soma Ufu.11:2).

Mwanamke,
yaani Wayahudi waisraeli watakimbilia jangwani ambapo watawindwa,
lakini hapa watakuwa chini ya ulinzi wake Mungu kwa
muda wa siku 1260
(soma Ufu.12:6). ·

Mpinga Kristo
atakuwa na uwezo na mamlaka makubwa kwa muda wa miezi 42
(Ufu.13:5).

Wateule 144,000 Tukio la muhimu sana wakati wa mwanzo wa dhiki kuu ni ufufuo kiroho utakaotokea kati ya wayahudi.

         Ufu. 7:4
yasema wazi kwamba kutakuwa na watenda kazi na
watumishi  144,000 kutoka taifa la Israeli ambao watakuwa na muhuri kwenye vichwa vyao:

"Na nikasikia nambari ya wale waliokuwa na mihuri
144,000 ya makabila yote ya Israeli walikuwa na mihuri"
(Ufu. 7:4).

Hakuna lile ambalo halieleweki kuhusu haya ambayo tumesoma hapa juu.

Ni kosa kusema kwamba ufufuo wa kiroho unaotajwa katika Ufunuo 7:1-8 utaletwa na kanisa au kikundi fulani maalum.

Somo hili lagusia taifa la Israeli.

Wakati huu,
Mungu atakuwa tayari amewaondoa wale walio na imani halisi kutoka hapa duniani.

Atawafufua wayahudi 144,000 kati ya wale ambao wamerudishiwa imani yao, au
wamemrudia Mungu na kupokea wokovu ili wawe mashahidi wake.

Ufunuo 7 yakubaliana na maneno ya unabii katika biblia ambapo kuna hakikisho
kwamba Mungu hatafufua tu taifa la Israeli na kuwarudisha hapa duniani, ila katika siku za baadaye watafufuka kiroho.

"Kwa hiyo waambieni nyumba ya Israeli, Bwana Mungu asema hivi:
sitendi hili kwa ajili yenu, Ee nyumba ya Israeli,
bali kwa ajili ya jina langu kuu, lililotiwa unajisi katika mataifa,
mlilolitia unajisi kati kati yao; nao mataifa watajua ya kuwa mimi ndiye Bwana,

asema Bwana Mungu,
nitakapotakaswa kati yenu mbele ya macho yao maana nitawatwaa kati ya mataifa,
nami nitawakusanya na kuwatoa katika nchi zote, na kuwarudisha katika nchi yenu wenyewe.

Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi,
nitawatakaseni uchafu wenu wote, na vinyago vyenu vyote.

Nami nitawapa ninyi roho mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu. Nami nitatoa moyo wa jiwe iliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.

Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi mtazishika hukumu zangu,
na kuzitenda.

Nanyi mtakaa katika nchi ile niliyowapa baba zenu,
nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu"
(Ezek. 36:22-28).

Leo hii kuna wayahudi wengi sana ambao wamepokea ujumbe wa
Agano Jipya unaohusu mwokozi wetu Yesu Kristo.

Hata hivyo wengi wao hawataki kuamua mara moja kumtambua kristo kuwa mwokozi na
wanafanya hivyo kwa ajili ya hofu kwamba huenda wakateswa na kupata taabu

au kwa ajili ya kutojua ni nini kitatokea pale wanapopokea wokovu.

Uamuzi utachukuliwa baada ya kunyakuliwa kwa wale walio na imani na wale
wayahudi wateule ambao tayari wamemkubali Kristo wamenyakuliwa pamoja na kanisa lote la Kristo.

Wale watakaoachwa itawabidii wafikirie kwa
makini kuhusu uamuzi wao utakaochelewa.

Kwa ajili ya matukio haya yote, idadi kubwa ya wayahudi kote duniani watanyenyekea na kutubu dhambi zao wakiongozwa na Roho Mtakatifu

na hapo kukubali kwamba Kristo ndiye Masihi.

      Ufunuo 7:3
Mungu atawachukua wateule wake 144,000
ambao ni watumishi wake waliowekewa muhuri pale mwanzo wa dhiki kuu, na yeye.

Wale walioachwa nyuma itawabidi wachunguze
upya msimamo wao.

Ev. Elimeleck nakukumbusha ya kwamba ktk siku hiyo au wakati huo wa dhiki kuu hakuna mzaha mzaha kama tulivyozoea leo na jana,

Tutatafutana lkn hali itakuwa mbaya mno kuliko.

Itaendeleaaa.......

         Fuatana nami
Ev. Elimeleck S Ndashikiwe