MAMLAKA YA KINYWA CHA MTEULE WA KRISTO.
-
Na Mwl Peter Mabula Mtenda kazi katika Shamba la Bwana YESU KRISTO
Mwokozi Bwana YESU KRISTO atukuzwe ndugu zangu wote.Karibu sana tujifunze
Neno la MUNGU ...
Thursday, 3 November 2016
KUREJEZWA KATIKA IMANI
" Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lolote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe."Wagalati 6:1
(1) Kosa lolote
Kosa lolote maana yake kosa lolote! Mtu akighafilika njia ya kufanya kwa wale walio wa Roho tu tunatakiwa kumrejeza upya katika imani, upya katika kosa husika na hatuambiwi sasa tuanze kusema na kuanza kumtangaza ovyo, "tulijua tu, yule kwa mwendo ule asingeweza kufika mbali..."
Hayo hayatarajiwi kufanywa na kuzungumzwa kwa "Walio wa Roho" hayo yatafanywa kwa wasio wa Roho maana ndio kinyume cha andiko hilo! Wasio/Walio wa Roho sio watu wa dhehebu fulani, ni mtu yeyote yule.
Katika andiko hilo haitajwi mtu ambaye hajawahi kukutana na Yesu! Hapo anatajwa mtu ambaye alikuwa katika imani na sasa amekengeuka ndio maana maandiko yanasema "Tunatakiwa kumrejeza upya.." Anayerejezwa ni mtu ambaye alikuwa katika mstari na sasa ametoka nje ya mstari, anatakiwa kurejezwa!
Wako watu wanaweza wakawepo makanisani lakini hawajawahi kukutana na Yesu, hawajahi kuokoka, wapo kwa sababu zao au kwa kufuata wazazi n.k. Hao andiko hili si la kwao! Andiko hili ni la mtu aliyekuwa katika njia salama na sasa hayupo amekengeuka huyo ndiye tunaagizwa kwa ajili yake, kumrejeza.
Ni vema tufanye hivyo! Tuache habari ya kukaa kaa na kuanza kumsengenya mtu, kama unajua mtu ameghafirika katika hilo unalolijua, tunatakiwa kumrejeza tena kwa roho ya upole na sio kujifanya sisi kama sasa ndio tumepatia pakusemea mambo yetu ya moyoni ya muda mrefu! Unamwambia mtu ambaye hata kuomba haombi, atasaidia nini huyo zaidi ya kusengenya tu. Aliyeghafilika muombee na huku ukijitahidi kumrejeza tena kwa roho ya upole kwa sababu kauli nazo zinaweza kumfanya mtu kuwa mbali zaidi! Lazima tuwe na kauli nzuri tunapotaka kumrejeza mtu!
(2) Ukijiangalia nafsi yako
Hapa tunaona katika maneno ya mwisho inasema "ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe.."
Pamoja na maagizo ya upendo ya kuwarejeza watu walioghafilika! Kuna tahadhari tunapewa! Tukiziangalia nafsi zetu tusije tukajaribiwa wenyewe; ako baadhi ya watu wanaruka la kwanza wanalifuata la pili! Hiyo haipo! Yaani wanadai wanaziangalia nafafsi zao kabla ya kujaribu kufanya la kwanza la kuwarejeza. Tunayakiwa kujiangalia nafsi zetu wakati tunafanya kazi ya kumrejeza aliyeghafilika! Hayo ni mapacha! Tunajiangalia nafsi zetu kwa maombi na umakini wa hali ya juu! Ili usije kujikuta unamvuta mtu kutoka shimoni kwa kamba, badala ya wewe kumvuta unavutwa wewe na kujikuta tumedumbukia shimoni sisi na kamba zetu! Hapo inakuwa hatari maana wote mkiwa shimoni huko mtatiana moyo chini kwa chini!
Ndugu zangu nawasihi sana! Ikiwa unajua mtu yeyote ameghafilika! Tusimuache kwa kusema "kila mmoja atalibeba furushi lake mwenye". Tuseme hayo baada ya kushindwa kumrejeza kwa jitihada zetu zote, ni kama tunahitimisha kazi yetu lakini tusiseme hayo tukiwa hatujafanya chochote kumhusu aliyeghafilika!
Tuko hivi wakati mwingine ni kwa neema ya Mungu tu, pamoja na jitihada zetu, lakini ni kwa neema ya Mungu pia! Angalia maisha yako! Maombi binafsi ni shida, lakini kinachotuufanya tusitetereke ni nini basi wakati maombi ni silaha yetu lakini hatuombi inavyotupasa? Tunaomba mpaka tukiwa kanisani tu au jumapili? Wako watu walikuwa waombaji lakini wamerudi nyuma, wako watu walikuwa na misimamo ya hatari lakini wamerudi nyuma!
Uwokovu ni safari ndefu sana! Ikitokea mwenzetu ameshambuliwa tumsaidie kadiri inavyowezekana, na kama tukishindwa basi tushindwe pia na kumzungumzia ovyo yaani tushindwe yote!
" BWANA nikumbuke mimi Marco Bashiri katika Ufalme wako, na kama unajua nitarudi nyuma! BWANA naomba ombi hili lipate kibali mbele zako! Uitoe roho yangu nisiendelee kuishi maana nitalitukanisha jina lako sana BWANA! Ni heri uniingize katika ufalme wako kabla ya wakati wangu"
" Ndugu zangu, mtu akighafilika katika kosa lolote, ninyi mlio wa Roho mrejezeni upya mtu kama huyo kwa roho ya upole, ukijiangalia nafsi yako usije ukajaribiwa wewe mwenyewe."Wagalati 6:1
#MTUWAVITA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)




Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na akaondoka kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki yangu aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu ili kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.
ReplyDeleteMwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwa ajili yangu - na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.
Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.
Lakini sio hivyo tu - Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyozunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.
Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote - huzuni, bahati mbaya, au kuchanganyikiwa - usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.
Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
dawnacuna314@gmail.com
Uchawi wa mapenzi wa Dkt. Dawn hufanya maajabu kweli.
ReplyDeleteNiliwasiliana na Dkt. Dawn wakati uhusiano wangu ulipovunjika kabisa. Mpenzi wangu wa zamani alikuwa ameniacha na kunizuia kwenye mitandao yote ya kijamii. Nilivunjika moyo na kupoteza tumaini. Baada ya kushauriana na Dkt. Dawn, kila kitu kilibadilika. Mpenzi wangu wa zamani alirudi peke yake, akaomba msamaha kwa dhati, na akaomba msamaha. Leo, tunaishi pamoja kwa furaha, na hata tuna mtoto.
Maneno hayatoshi kuelezea jinsi ninavyoshukuru. Kutokana na uzoefu wangu, naweza kusema kwa ujasiri kwamba Dkt. Dawn ni halisi, anayetegemewa, na mwenye nguvu. Ikiwa unakabiliwa na hali yoyote ngumu maishani mwako hivi sasa, Dkt. Dawn anaweza kukusaidia.
ANAWEZA KUKUSAIDIA KWA MATATIZO YAFUATAYO:
Kurudisha ndoa na mahusiano yaliyovunjika
Kuvutia mafanikio na ukuaji katika biashara
Matatizo ya uanaume, utasa, na ukosefu wa watoto
Kurejesha mali zilizoibiwa au zilizopotea
Kurudisha kazi zilizopotea au fursa za kazi
Kinga dhidi ya uchawi na macho mabaya
Hirizi za mvuto
Kutatua migogoro ya ardhi na mali
Kuwafanya wapenzi kutimiza ahadi zao
Kushinda kesi mahakamani, na mengine mengi
Huu si ulaghai — ni ushuhuda kutoka kwa uzoefu.
Kwa maelezo zaidi, wasiliana naye moja kwa moja kwenye WhatsApp. +2349046229159
dawnacuna314@gmail.com